UWEZO WA KUTAWALA
NA
KUMILIKI ARDHI/NCHI
KWA NJIA
YA
MAOMBI

NA MWL. NICKSON KIPANGULA

MFUMO WA KIROHO UNAOTOA KIBALI CHA KIFALME
              
                  Dhana ya ufalme imeanzia katika kitabu cha MWANZO 1; 28
Inasema, “ Mungu akawabarikia (akaachilia NGUVU) , Mungu akawaambia, zaeni (be fruitful), mkaongezeke( multiply), mkaijaze nchi na KUITIISHA; MKATAWALE samaki wa baharini, na ndege wa angani, NA KILA kiumbe CHENYE UHAI kiendacho juu ya nchi (LAND).”.
Vipo vitu vya kujifunza hapa;

1.      Kumbe lengo kuu la Mungu kumuumba mtu ni kuwa aweze kutawala na kutiisha NCHI pamoja na kila kiumbe ili mradi kipo ndani ya nchi.
Ø  KUMBUKA mtu ni roho, anayo nafsi , na anaishi ndani ya mwili. MAANA YAKE hayo maagizo yote anaachilia kwa roho ambayo baadaye ataiumbia mwili .
2.      Pia anaposema, AKAWABARIKIA maana yake AKAACHILIA NGUVU ya kufanya kile ambacho anawapa kukifanya ambacho ni KUTAWALA na KUTIISHA.
Ø   Maana yake bila NGUVU huwezi kutawala na kutiisha chochote.
3.      KUTAWALA NA KUTIISHA hii ni dhana ya ufalme.
Ø  KUMBUKA kiongozi yeyote anaweza kutawala kwa maana ya kuongoza lakini MFALME pekee ndiye anaweza kutiisha KWA MAMLAKA aliyonayo.
4.      Suala la kuzaa halipo tu katika dhana ya watoto kwenye biblia za kiingereza imeandikwa, BE FRUITFUL. MAANA YAKE zaeni matunda.
Ø  Kwa tafsiri nyingine ni kwamba ndani ya mtu ameweka MBEGU(SEEDS) na kuachilia nguvu (BARAKA) ya kuzaa au kutoa matunda sawasawa na Mbegu ambayo ameweka.
5.      Kumbe kila kiumbe chenye uhai  kinatawaliwa na kutiishwa na mtu.
Ø  Na sio tu chenye uhai ili mradi kinaunda nchi (land) kimepewa mtu awe mtawala na mtiishaji wake. Mfano bahari, mito, mawe, milima, upepo, mvua, jua, N.K
6.      KUTAWALA na KUTIISHA kupo katika ulimwengu wa roho maana yake kunatumia MFUMO WA KIROHO WA KIUTAWALA na ndiyo maana anawasemesha Adamu na hawa kabla ya kuumba miili yao, punde tu baada ya kuumba roho zao.
UFALME ni milki/mali ya mfalme, eneo ambalo lina mipaka kamili (territory) na lina mfumo Fulani wa kwake kiuchumi, kiutamaduni na kimila pamoja na Ibada.  Ndani ya ufalme kuna watu ambao wanatawaliwa na mfalme ambao inawezekana ni raia (citizen) ama watumwa.
MFALME ni Yule ambaye ufalme upo chini yake maana yake anayemiliki huo ufalme, watu na kila kilichomo ndani ya huo ufalme.
Ukiisha itwa ufalme lazima kuna mfalme. Ukipewa ufalme maana yake wewe ni mfalme katika eneo hilo.
LUKA 12;32, “Msiogope enyi kundi dogo, kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule UFALME”.  Kwa tafsiri nyingine anasema kwa kuwa baba yenu ameona vema kuwapa ninyi kuwa wafalme katika eneo hilo la ufalme.
Mfalme hatawali kwa kutumia mawazo ya wengi, mijadala,ama mapendekezo ya raia wake ama viongozi wengine wafanyavyo. MFALME anatawala kwa KUTUMIA NENO/AMRI.
Wakati Yesu amepigiliwa misumari msalabani PILATO aliweka kibao juu ya Msalaba kisemacho, “YESU MNAZARETI,  MFALME WA WAYAHUDI”. Wapo watu walipinga na kushauri kibao kitolewe lakini Pilato kwa Mamlaka ya Kifalme akawaambia “NILIYOANDIKWA NIMEYAAANDIKA”. ( YOHANA 19;19 – 22 ).  Hiyo ni Amri/neno la kifalme, na tunaona hakuna mtu  aliyeendelea tena kubisha bisha.

Mungu anatawala kifalme ndiyo maana hata katika uumbaji tunaona anaamuru kwa kusema IWE NURU – INAKUWA ,NA LIWE ANGA KATIKATI YA MAJI… - LINAKUWA, NCHI IZAE KIUMBE HAI… - INAZAA N.K.  huu ndio mfumo wa kifalme. Unatumia NENO na AMRI siyo ombi na hakuna namna NURU itasema ooh subiri kwanza… au sitaki… n.k.
MHUBIRI 8;4, “ kwa kuwa NENO LA MFALME lina NGUVU, naye ni nani awezaye kumwambia huyo wafanya nini?”

Mfalme akiisha kuongea maana yake ametoa maamuzi ya mwisho ambayo hayawezi kuhojiwa na yeyote wala kujadiliwa kwa dhana ya kupinga. Ndiyo maana KWA MUNGU tu kuwa mfalme kunaondoa dhana ya kujadili au kurekebisha NENO LOLOTE ambalo amelisema kwa kinywa chake. Hata kama kwako halikupendezi ama unaona gumu kulifuata.
Mfumo wa kiutawala ambao Mungu ameuweka asili ni kwamba YEYE ATAWALE MBINGUNI NA DUNIANI na mwanadamu atawale DUNIANI. Maana yake Mungu amekusudia atawale duniani kupitia mwanadamu aliyemuumba na kuweka kwa kutumia neno/amri ya Mungu.
UUNGU ni UFALME ndiyo maana baada ya mwanadamu kumkabidhi shetani nafasi ile, shetani akaitwa mungu wa dunia hii. Nafasi ambayo alikuwa nayo mwanadamu kabla ya kuasi.
Soma ZABURI 82; 6, “ Mimi nimesema , ndinyi miungu, Na wana wa ALIYE JUU , nyote pia”.
Pia katika ZABURI 115;15-16, “Na mbarikiwe (MPEWE NGUVU) ninyi na BWANA, aliyezifanya mbingu na nchi. MBINGU NI MBINGU ZA BWANA bali nchi AMEWAPA WANADAMU.”
MAANA YAKE Mungu ndiye aliyeifanya mbingu na nchi lakini kwa namna ya utawala ameamua amkabidhi mwanadamu kama mfalme aisimamie, aitawale na kuitiisha. Ndiyo maana yeye anaitwa mfalme wa wafalme, maana yake wewe ni mfalme lakini yeye ndiye mkuu wako. NDIYO MAANA UNATAWALA KIMAMLAKA KWA KUTUMIA NENO LAKE na siyo NENO LAKO.
Baada ya mwanadamu kuupoteza ufalme aliopewa na kumkabidhi shetani kwa sababu ya udhaifu, Mungu akaandaa Mfumo mpya wenye nguvu wa kumuuingiza mwanadamu katika UFALME JUU YA DUNIA kwa namna ya kiroho tena.


UFUNUO 5;9-10, “ Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewekukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa (kusulibishwa au kufanyika sadaka ya kuteketezwa), ukamnunulia Mungu kwa Damu yako watu wa KILA kabila,na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa UFALME na MAKUHANI kwa Mungu wetu; nao WANAMILIKI JUU YA NCHI”. Sema tena …”NAO WANAMILIKI JUU YA NCHI..”
Kumbuka nimekuambia kuwa ANAYEMILIKI NI MFALME PEKEE.
Na mfumo ambao Mungu ameuweka wa mwanadamu kumiliki juu ya nchi ni kwa njia ya UFALME NA UKUHANI.
Inawezekana unajiuliza kwa NINI UKUHANI UKAINGIA HAPO????. SIKILIZA; UMILIKI ambao Mungu ametupa ni kwa njia au namna ya Kiroho.  UKUHANI unafanya kazi ya utakaso au toba ili kuweza kuunganisha MBINGU na NCHI/ARDHI ya eneo lolote ambalo umepewa kumiliki.
NDIYO MAANA unabaki kusema, nimeambiwa kila nitakapokanyaga nimepewa kumiliki mbona ninateswa na nchi na vilivyomo?? Mbona ardhi inanizalia miiba na michongoma???? Mbona wachawi wananimiliki??? SUALA hapa sio kukanyaga suala hapa ni je, UNAKANYAGAJE???. LAZIMA ukanyage mkanyago wa KIKUHANI kwanza, yaani toba juu ya ardhi hiyo na BAADAYE mkanyago wa KIFALME kusema neno la kifalme kwa kutumia NENO LA MUNGU juu ya huo ufalme au nchi/ ardhi unayotaka umiliki na kutiisha.
Danieli Mbali na kuwa ni mtoto wa Mungu alijikuta katika wakati mgumu ambapo maombi yake anayoomba hayana majibu, ni mpaka alipoingia kwenye maombi ya siku  21 ya kuunganisha Mbingu na ardhi aliyopo. KUMBUKA Wakati huo Danieli yupo utumwani maana yake siyo katika ardhi anayoijua.Kwa maana hiyo yupo kwenye ardhi ya uovu maana inamilikiwa na utawala wa mataifa wasiomjua Mungu.  DANIEL 10;1-13.


Fahamu Ardhi ya eneo inapomilikiwa na adui kunakuwa na kukatika kwa mawasiliano ( TOTAL DISCONNECTION) kati Ya Mbingu na ARDHI/ NCHI. Muunganiko wa Baraka za Mungu au majibu ya kimungu kukufikia unakuwa ni mgumu sana kwa maana MKUU WA ANGA(PEPO) anatawala kutokana na kibali kutoka hapa chini ardhini/nchi na siyo kwamba anapata kuzimu  no, no ,no. maana yake kukiwepo na mfalme ambaye ni wa kuzimu, Mkuu wa anga atatawala na kukiwepo na mfalme ambaye ni wewe katika hilo eneo maana yake anga lake litakuwa na Malaika.
 Madhara ya mkuu wa anga kutawala anga ni kuwa anakuwa na uwezo wa kuzuia kila jambo jema linaloachiliwa kutoka mbinguni na pia anakuwa na uwezo wa kuachilia mabaya juu ya nchi kwa kushirikiana na mawakala wengine wa shetani. Vile vile, Wachawi, mapepo, majini, waganga wa kienyeji, mizimu n.k vinapata uhalali wa kutawala eneo na watu wa eneo na kulitumia kwa kupata KIBALI kutoka kwa mkuu wa anga la eneo lile ambaye naye anapata fursa ya kutawala kutoka kwa mfalme aliyepo katika ardhi/nchi hiyo husika.
Kilichomfanya Yesu akubali Kutoyatoa mapepo ya mtu wa nchi ya Ugerasi nje ya mji siyo kwa kuwa Yesu anayatii mapepo la hasha,, ni kutokana na SHERIA YA UFALME, maana yake wao walikuwa na uhalali wa kumiliki lile eneo ndiyo maana wakasema hata kama ukitutoa kwa huyu mtu tunaomba usitutupe shimoni (usitutoe mipakani mwa hii nchi) afadhali turuhusu tuwaingie nguruwe wale, na kwa kuwa wapo kwenye miliki yao akawaruhusu.
Na ndiyo maana utakuta kwamba Yesu baada ya kumfungua mtu Yule hakukubali Yule mtu afuatane naye kwa kuwa anataka ampe kazi katika nchi/ardhi yake ya kumiliki, kutiisha na kuondosha ufalme wa giza katika nchi/ ardhi yote ya Ugerasi.




Tusome LUKA 8;37-39, “ Na jamii ya watu wa nchi/ ardhi ya Wagerasi iliyo kando kando walimwomba (YESU) aondoke kwao, kwa kuwa walishikwa na hofu nyingi……[ yawezekana wakajua kaja huyu sasa mifugo yetu kwisha habari yake,,, maana yale mapepo ni mwendo wa kuzunguka mara kwa nguruwe, mara itakuja kwa ng’ombe baadaye kwa mazao ya shamba n.k ili mradi tu yana uhalali wa kukaa katika nchi ile]. Na mtu Yule aliyetokwa na pepo alimwomba ruhusa afuatane naye; lakini yeye alimwaga akasema, Rudi nyumbani kwako UKAHUBIRI yalivyo makuu Mungu aliyokutendea. Akaenda zake, akihubiri KATIKA MJI WOTE,  yalivyo makuu mambo aliyotendewa na Yesu”.


NAMNA AMBAVYO NGUVU ZA MUNGU NDANI YAKO ZINAVYOKUSAIDIA KUTIISHA KILA KITU KATIKA NCHI/ARDHI

Katika sehemu ya kwanza tumeona kidogo maana na tafsiri ya UFALME NA FALME, na mwanzo wa ufalme wa Mungu aliompa mwanadamu na alivyoupoteza na kuukabidhi kwa shetani, hatimaye Yesu kuurejesha tena.
Pia tukaona kidogo juu ya uhusiano wa Ardhi na Mbingu pamoja na Anga. Sasa ,tusogee kidogo;
Tukisoma Efeso 3;20 inasema, “ Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya MAMBO YA AJABU MNO kuliko YOTE tuyaombayo au tuyawazayo,  KWA KADIRI ya NGUVU itendayo kazi NDANI YETU;”

Hapa anachokisisitiza mtume Paulo ni hiki; Utendekaji wa mambo ya ajabu mno haufanyiki kwa kutegemea kiwango gani cha maombi unafanya ama kiwango gani cha IMANI(…TUYAWAZAYO…) ulichonacho la hasha. UTENDAJI WA MAMBO YA AJABU MNO unategemea na KIWANGO CHA NGUVU YA MUNGU KILICHOMO NDANI YAKO.
Ndiyo maana tuliona katika kitabu cha Mwanzo kuwa BARAKA maana yake NGUVU na anaposema Mungu akawabarikia maana yake Mungu akaachilia nguvu ambazo zitawapa kiwango cha uwezo wa kutawala na kutiisha nchi na vilivyomo.
Hii ndiyo siri iliyomfanya Yesu awe anashinda muda mwingi mlimani akimwomba Mungu. Watumishi wengi huomba kwa mzigo pale tu wanapokuwa na huduma, semina ama mkutano wa injili. Matokeo yake anajikuta anaishiwa nguvu mapema. Yesu haikujalisha mchana atakuwa na huduma ama hana huduma, jioni lazima apitie mlimani kuomba. Na cha ajabu ni kuwa  hakuna mwanafunzi anamwambia Yesu leo twende pamoja basi!!!!.
Wanamshangaa tu kuwa duh, hata upepo na mawimbi ya bahari vinamtii?? Suala halikuwa kwamba IMANI tu la hasha, SUALA NI ILE NGUVU YA MUNGU NDANI YAKE inayokusanywa kwa njia ya maombi ndiyo ilimfanya atembee juu ya bahari, afufue wafu, aponye vipofu,viwete n.k.
Kutembea juu ya maji , kufufua wafu, kuponya wagonjwa, kutoa pepo kwake Yesu halikuwa ni jambo la ajabu wala kuita muujiza la hasha, Yalikuwa ni maisha yake ya kawaida sana ya kila siku kwa kuwa alijua kutafuta na hatimaye kutumia nguvu ya Mungu iliyomo ndani yake kutawala na kutiisha nchi na kila kilichomo.
Mfumo ambao Mungu ameuandaa kwa namna ya kimawasiliano kati yako na ulimwengu wa roho  ni maombi. Maombi ndiyo yanayoachilia Nguvu za Mungu kukuwezesha kutawala na kutiisha.
KWA MUNGU –  unafanya maombi,,,,, KWENYE VITU –  unaachilia nguvu ili kifanyike chochote unachotaka kifanyike. Maadamu Kiwe ndani ya Mamlaka ya Neno la Mungu (maana yake NENO LA MUNGU liwe limejieleza kuwa na uwezo/UHALALI wa kufanya hicho kitu).
PASIPO MIMI, NINYI HAMWEZI NENO LOLOTE,, YOHANA 15;4-5.. Maana yake USIPO KUWA na Nguvu za Mungu ndani yako kupitia Maombi ningumu sana kuuendesha utawala waadui katika ardhi au eneo ulilopo.

ISAYA 37;3 – 4, “ Wakamwambia, Hezekia asema hivi, Siku hii ni siku ya dhiki, na aibu na matukano; maana watoto wa tayari kuzaliwa, wala hapana NGUVU ya kuwazaa. Yamkini BWANA , Mungu wako, atayasikia maneno ya huyo amiri ambaye mfalme wa Ashuru, bwana wake, amemtuma ili amtukane Mungu aliye hai; na BWANA, Mungu wako atayakemea maneno aliyoyasikia; basi inua DUA yako kwa ajili ya mabaki yaliyobakia.”
Mfalme Hezekia amepewa milki ya eneo la Yerusalemu kwa Namna ya kiroho na Kimwili. Inafika mahali anakuta maadui wanawapiga na kuwararua na mbaya zaidi anashangaa mpaka Amiri wa Mfalme wa Ashuru anathubutu kumtukana Mungu Lakini Mungu yupo kimya. Amesahau kuwa Mungu anatawala dunia kupitia mwanadamu na Shetani anatawala dunia kupitia mwanadamu.
 HAKUNA ROHO YOYOTE ITAKUWA NA UHALALI WA KUTAWALA AU KUFANYA OPERATION YOYOTE KATIKA DUNIA BILA KUPITIA MWANADAMU. Na  ndiyo maana Hata shetani alipotaka kupata umiliki halali wa dunia alimtumia Mwanadamu katika bustani ya Edeni. Vile vile baada ya kuona Yesu amefanikiwa kupewa mwili ili apate uhalali wa kutawala na kumiliki Dunia na hatimaye amkabidhi huo ufunguo wa utawala na umiliki mwanadamu ( kanisa) , alijaribu kumlaghai Yesu mapema Kuwa ukinisujudia nitakupa vyote ili amwangushe mkenge akashindwa na ndiyo maana hatimaye Yesu akamnyang’anya ufunguo wa MAUTI na kuzimu na kulikabidhi kanisa ( MATHAYO 16;18 -19 ) na akaandaa sheria  (WARUMI 8;1 -2 ).
Sasa huyu Mfalme Hezekia anapogundua kuwa Mungu hawezi ingilia kati vita hiyo hata kama anatukanwa na watu wake wanaangamia. Lazima atumie mtu Fulani ili ajipatie uhalali wa kuporomosha mashambulizi kwa Mfalme wa Ashuru. Anamwomba Isaya ainue dua kwa Mungu ili kuachilia NGUVU za kuwazaa watoto (USHINDI DHIDI YA ASHURU) na kwa ajili ya mabaki yaliyosalia.
Kumbuka hawa ni Israeli taifa la Mungu lakini wanajikuta ardhi yao imetekwa na Mfalme wa Ashuru na kwenye maono, ndoto, n.k wanaona kabisa ni milki yao kwao lakini katika uhalisia au uliwengu wa mwili wanajikuta bado wapo chini ya milki ya adui.

Katika Isaya 40;30-31, “ Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume  vijana WATAANGUKA, bali WAMNGOJEAO ( WAMWOMBAO/WAMTAFUTAO) BWANA watapata NGUVU MPYA; Watapanda Juu Kwa Mbawa Kama Tai; Watapiga Mbio, Wala Hawatachoka; Watakwenda KWA MIGUU Wala Hawatazimia.”
·         Kinachofanya vijana wazimie ni kukosa NGUVU ( YA MUNGU) ya kiwango Fulani ambayo ingewafanya wakabiliane na mazingira mapya wanayokutana nayo.
·         Wamngojeao BWANA  watapata NGUVU MPYA. Maana yake katika kila hatua au jambo lolote linalowakabilii wanapata NGUVU INAYOZIDI mazingira hayo kiasi kwamba wanapata uwezo wa kumiliki na kutiisha KILA  mazingira yaliyopo mbele yao.
KURUKA JUU KAMA TAI MAANA YAKE:-
1.      Kuwa juu ya uwezo wa adui na hivyo kufanya urahisi wa kupambana naye
2.      Kupata fursa ya KUONA kila kinachoendelea chini ya ardhi na kujua hazina zako zilizofichika katika Ardhi kwa namna ya kiroho. NDIYO SABABU anasema utapata NGUVU MPYA maana yake  siyo kama ile ya nyuma katika ukuu wake.
Yesu alipowatuma wanafunzi kuhubiri tunaambiwa WALITOA PEPO mpaka wakaja kumsimulia Yesu. Lakini kuna siku nyingine Yesu amepanda mlimani kuomba na baadhi yao. Wale waliobaki haohao WAKASHINDWA KUMTOA PEPO. Sababu kuu ni kuwa ndani yao kwa wakati huo HAKUKUWA NA NGUVU inayozidi uwezo wa ile Mizizi ya pepo la kifafa kufanya litoke. Na tunaona Yesu anawaambia NAMNA HII/STAILI HII/ NGUVU HII( ndani ya pepo) haiwezekani kutoka isipokuwa kwa KUFUNGA NA KUSALI.
Hapo anataka awaeleweshe kuwa sababu si kuwa yeye ni MWANA WA MUNGU ndiyo maana kaweza kutoa pepo la hasha, Wala si suala la kiwango chao cha imani na ndiyo maana akasema mbona hata mngekuwa na  IMANI kama SIZE ya punje ya HARADALI mngeweza Kuuambia mlima huu ng’oka hapa uende baharini nao ungetii. Mathayo 17;20b-21.Lakini anawaambia kilichomsaidia ni kwa sababu AMEFUNGA NA KUOMBA(AKAPATA NGUVU) ndiyo maana kaweza kumtoa Pepo la kifafa.

Kuna mahali pengine anawaambia kuwa, mwanzo nilipowatuma,  niliwaambia msibebe mkoba wala kanzu wala panga, LAKINI SASA HIVI mwenye kanzu mbili amgawie mwenzake hali kadhalika mwenye panga pia. ( Hapo alikuwa anazungumzia kwa namna ya ROHONI kuwa wajipange kimaombi kwa sababu mbele yao kuna upinzani mkubwa kuliko nguvu walizoenda nazo kwenye huduma iliyopita. NDIYO MAANA anasisitiza wakeshe pamoja naye. Na hata yeye akiwa anaomba tunaambiwa malaika akaja akamtia NGUVU. LUKA 22;35 – 46.
MITHALI 24;10, “ UKIZIMIA siku ya taabu, NGUVU zako ni chache”.
Pia katika  ZABURI 105;4, “anasema Mtakeni BWANA na NGUVU ZAKE, utafuteni uso wake siku zote.”
Ukitumia MUDA MWINGI kukaa na Mungu na kutaka NGUVU ZAKE itakusaidia sana kukufanya kutumia muda mchache kutoa pepo, kuponya wagonjwa, kufufua wafu, kumiliki na kutiisha n.k
Ukikaa kwenye maombi kwa dakika tano,kumi utakesha na pepo kwa masaa matatu ,kumi hadi siku kadhaa na sauti kukukauka. Bali ukikaa muda mwingi na Yesu na kutaka NGUVU ZAKE, utatumia SEKUNDE CHACHE kutatua tatizo lililopo katika ulimwengu wa roho na wa mwili na pia kuamrisha kila kilicho kinyume chako.
YAFANYE MAOMBI KAMA NI SEHEMU YAKO YA RATIBA NA MAISHA YA KILA SIKU NA SIYO KUFANYA KUWA NI TUKIO MAALUMU. MUNGU ANATAMANI MARA NYINGI KUZUNGUMZA NA SISI, ANAHITAJI FURSA YETU KUPITIA MAOMBI NA ANATAMANI AENDELEE KUTAWALA NCHI NA KILA KILICHOMO KUPITIA WEWE.
OMBA MUNGU AKUPE NGUVU NA KIU YA MAOMBI , UWEZE KUMILIKI NA KUTIISHA.


UHUSIANO ULIOPO KATI YA MADHABAHU NA UHALALI  WA KUMILIKI NA KUTIISHA ARDHI / NCHI ULIYOPO

Madhabahu ni mahali ambapo sadaka ya kuteketezwa (DHABIHU) inatolewa. Pia ni mahali mahususi pa Mungu kusemezana na Mwanadamu na kuhojiana na vile vile ni mahali panapo pokea muachilio wa Baraka za Mbinguni ( kutoka kwa Mungu) kumfikilia Yule ambaye anahusika au kuihudumia hiyo madhabahu.
Mahali popote ambapo kunafanyika ibada kuna madhabahu,, maana yake, kanisani, nyumbani, ardhini, makaburini, ndani ya mwanadamu, maporini, kwenye mawe na kadhalika. Madhabahu ni moyo wa hilo eneo hilo. Maana yake madhabahu  ya nchi ni moyo wa nchi. MOYO wa mwanadamu kwa mfano  unafanya kazi ya kuachilia damu, chakula na hewa kwenda sehemu nyingine zote za mwili. Pamoja na hilo hukusanya kila aina za uchafu kutoka maeneo mbalimbali na kuupeleka unakohusika ili kutolewa nje ya mwili. Moyo ni kiungo cha muhimu na ndiyo maana katika ulimwengu wa roho ni bora mtu aweke jambo ulilo mfanyika kwenye akili yake kuliko aweke moyoni.
Mithali 4;23, “LINDA sana MOYO wako kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima”.
Chemchemi za uzima maana yake kila kinachohusu uzima ndani yako kinaachiliwa kutoka kwenye moyo na kusambaa kuweka uzima maeneo yote yakuhusuyo.
Madhabahu ndiyo yanayohusika kuachilia uzima fulani katika eneo ambalo yamewekwa. Madhabahu inatoa kibali cha Ibada ya kimungu au ya kishetani kufanyika.




Tulikuwa kwenye kanisa moja na marafiki zangu wa kiroho, Mungu akanisemesha juu ya madhabahu ya kanisa lile na jinsi ambavyo shetani amebadilisha na kuruhusu Ibada za kishetani, kafara za watoto wachanga, na kadhalika kufanyika. Tulikuwa na maombi juu ya kukomboa nyakati za vijana zilizotekwa.
Na katika kanisa hilo wazee tu ndo walikuwa washiriki wa Ibada mbalimbali hususani fellowship n.k. tukaingia kuomba toba juu ya ile madhabahu na kuvunja kila pando la adui na kufuta uhalali wa shetani na mawakala wake kutumia. Baada ya hapo kukafuatiwa na Semina. Yaani ilifikia mahali wazee Fulani wakaanza kulalamika na kusema hawa vijana wanataka kupindua kanisa.Yesu alitenda, mpaka sasa vijana ndo wengi kwenye ibada za pale na baadhi ya wazee hatuwaoni tena. Hususani ambao shetani aliwaweka makuhani kwenye madhabahu ile.

Madhabahu inafanya kazi ya kuachilia vitu vya mungu wake kwa watu na pia inakusanya malemeo ya hao watu na kutumia mifumo Fulani kutupa nje. Kuna vitu ambavyo Mungu akiachilia ni lazima vipitie pekee katika Madhabahu ili vikufikie la sivyo, vinakwama. Kama ilivyo kwenye moyo.
Katika Mwanzo 12;1 – 9, anafafanua uhalali wa kumiliki kwa uwepo wa madhabahu
Tunasoma, “ BWANA akamwambia Abramu, TOKA WEWE KATIKA NCHI YAKO, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonesha nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako, nawe uwe Baraka……………………................BWANA akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko AKAMJENGEA MADHABAHU BWANA aliyemtokea. Kisha akaondoka huko akaenda mpaka mlima ulio upande wa  mashariki wa Betheli, akaipiga hema yake; alikuwa na Betheli upande wa Magharibi, na Ai upande wa mashariki, AKAMJENGEA BWANA MADHABAHU huko ,akaliitia jina la BWANA.
Ukisoma sura ya 12 na ya 13 katika kitabu hiki cha Mwanzo utaona kila mahali Mungu anapomkabidhi Abramu kumiliki, Abramu anajenga madhabahu. Hii ni kwa sababu anajua fika kwamba madhabahu ndiyo ambayo inampa uhalali way eye kumiliki mahali hapo haijalishi kuna wageni wa aina gani na wenyeji mahali hapo.

MADHABAHU INAPEWA UHAI KWA SADAKA YA KUTEKETEZWA ( DHABIHU) bila hivyo madhabahu inabaki ni jengo tu. WARUMI 12;1

1WAFALME 18;21 – 46 hapa tunamuona Eliya akiwa na manabii wa mungu baali na tunaona anatafuta kibali cha kujenga madhabahu kiaina. Lengo la Eliya ukisoma vema utaona sio kushindanisha miungu na Mungu ila ilikuwa ni kutafuta mlango wa kupata kibali cha kujenga madhabahu ya Mungu aliye hai, na ndiyo maana unakuta anaweka mawe 12 ili kuunganisha makabila yote kumi na mbili ya Isrraeli kwa madhabahu ile. Na ili kuifanya madhabahu kuwa hai Eliya anaomba kuandaliwa ng’ombe kama dhabihu ili aiteketeze kw moto juu ya madhabahu. Na baada ya shughuli zote unakuta baada ya hapo anamwambia Mfalme Ahabu kuwa INUKA ULE UNYWE, MAANA KUNA SAUTI YA MVUA TELE. Kumbuka ni mvua ambayo Eliya nabii aliizuia kwa Neno la BWANA  isinyeshe kwa zaidi ya miaka mitatu. Sasa, ili mvua ile inyeshe tena juu ya nchi yao lazima iwepo madhabahu ya kimungu kuruhusu mvua hiyo kunyesha. Kwa tafsiri nyingine Eliya anatafuta uhalali wa kumiliki ile ardhi /nchi kupitia ile madhabahu atakayo ijenga ili kuwepo na muachilio wa Baraka ya mvua tena juu ya ardhi hiyo.

KUMBUKA nilikuambia kuwa; Madhabahu ndiyo inatoa uhalali wa umiliki wa ardhi, na ardhi ikimilikiwa na adui inasababisha TOTAL DISCONNECTION( MTENGANIKO) kati ya ardhi hiyo na Mungu, na kunapotokea hivyo anga la hiyo ardhi linakuwa linamilikiwa na MKUU WA ANGA(PEPO). Na kazi yake kuu ni KUZUIA kila kinachoachiliwa kama Baraka au majibu ya maombi ya watakatifu Mbinguni na pia kutoa kibali cha ufalme wa giza kufanya kazi juu ya ardhi na watu na kila kitu juu ya ardhi hiyo iwe ni wachawi, ibada za kipepo, baa, miungu, kafara, vikao vya kipepo n.k. Shetani anapata kibali/ uhalali wa kuachilia magonjwa, vifungo, roho za umasikini, ukichaa, kuvuruga ndoa za watu, kuteswa na majinamizi usiku, roho za ajali, vifo vya ghafla,utoaji mimba, kafara, kufelisha masomo n.k. DANIELI 10;3,13
Hapa huyu malaika anasema , ……. “ tazama huyo mikaeli ,mmoja wa hao wakuu wa Mbele, akaja kunisaidia; NAMI NIKAMWACHA HUKO PAMOJA NA WAFALME WA UAJEMI”.
Maana yake bado vita inaendelea nah ii ni kwa sababu hawa wafalme au wakuu wa anga la uajemi bado wanadai uhalali wao juu ya ile ardhi kwa maana hakuna madhabahu danieli ameijenga kwa sadaka mahali pale.  Ingawa Katika SURA YA TISA YA KITABU CHA DANIELI tunaona Danieli akiomba toba juu ya ardhi na watu wa Israeli na mlima mtakatifu wa MUNGU yaani madhabahu,, maana yake anaondoa madhabahu na mapando juu ya ardhi yao ya kipepo lakini hatuoni mahali akitoa Sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ili kuachilia UHALALI wa umiliki wa ardhi ile juu yao.
Shetani akijenga madhabahu katika eneo la shule haijalishi walimu wanafundishaje na wanafunzi wanajituma vipi, roho ya kufeli itawasumbua sana wanafunzi HATA WALIOOKOKA ( WATEULE). Madhabahu ya shetani ikikalia nchi haijalishi uongozi ni mchapa kazi vipi au mfumo wa kiutawala ukoje. Lazima hata hivyo ataachilia vitu vya kwake. Kiongozi awe mzuri kiasi gani hawezi kuzuia ajali kutokea, hawezi zuia vifo mbalimbali kutokea, hawezi kuzuia majanga na balaa katika nchi, hawezi zuia uchumi usishuke. Ni madhabahu peke yake juu ya nchi ndiyo inayo achilia au kuzuia mabaya kutegemeana na aina ya mungu wa madhabahu hiyo.
Ndiyo maana neno linasema kama MISINGI IKIHARIBIKA( MF. MADHABAHU YA MUNGU ) mwenye haki atafanya nini???. Zaburi 11;3.
Tutaomba wee kwaajili ya familia, mashule na vyuo, nchi, makazi, ajira, ndoa, biashara n.k lakini tusipojua msingi wa kimadhabahu katika maeneo hayo ulivyo na kujenga madhabahu ya kimungu, tutakuwa tunajilisha upepo.
Kumbuka; unapobomoa, kuharibu na kuangamiza jua pia kuna kujenga na kupanda. Usiishie tu kuvunja na kuharibu madhabahu za giza(shetani) bali pia kumbuka zaidi KUJENGA NA KUPANDA madhabahu ya Kimungu katika jina la Yesu. Yeremia 1;10.
2 nyakati 1;6 – 7, “… Suleimani akaipandia huko madhabahu ya shaba mbele za BWANA , iliyokuwako hemani pa kukutania, akatoa sadaka elfu za kuteketezwa ( DHABIHU) juu yake. Usiku ule Mungu akamtokea Sulemani, akamwambia, OMBA UTAKALO NIKUPE”.
Hapa tunaona kilichompa uhalali na kibali Sulemani cha kuambiwa kuomba analotaka (LOLOTE) ni madhabahu iliyotiwa uhai kwa sadaka aliyotoa na ndipo akapata muachilio wa aina zote za Baraka atakazo zitaka. Mara ngapi Mungu anasema na wewe omba utakalo nami nitakupa???. Kuna mambo mengine hayaendi bila yaw ewe kuihudumia madhabahu. Tukisisitiza utoaji kanisani au katika huduma unahisi kuwa hawa watumishi siyo bure, wanataka walee pesa zetu ama vitu vyetu, bila kujua kuwa unafuta uhalali wa Mungu kukumilikisha ardhi yako kupiitia madhabahu. YAANI NIKWAMBIE ukiihudumia vema madhabahu (KWA SADAKA YA KUTEKETEZWA INCLUDING MWILI WAKO [ WARUMI 12;1]) unafanya Mungu akose namna atalazimika tu kukwambia sema lolote( Mali, utajiri, mume/mke, watoto, kazi, cheo, ufaulu, uponyaji, kufunguliwa, n.k) name nikupe. NA HAKIKA YAKE ATAKUPA. Maana huo ndiyo mfumo aliouweka wa muachilia wa chochote kwako mwanadamu
Lakini kumbuka pia PASIPO IMANI haiwezekani kumpendeza Mungu, Maana kila amwendeaye Mungu LAZIMA (SIYO HIARI) aamini kwamba yeye yupo na kwamba HUWAPA THAWABU wale wamtafutao. WAEBRANIA 11;6.
Usitoe mchango wa jengo, toa sadaka ya jengo, Usitoe Mchango wa Maendeleo ya Dayosisi toa Sadaka ya maendeleo ya dayosisi, UNANIPATA SAWASAWA????
Makanisa mengi yanatumia neno mchango kwenye sadaka mbalimbali ndiyo maana watu hulalamika kuwa duh leo siendi kanisani michango imezidi. Lakini ungekuwa unatoa kama Sadaka usingekuwa unalalamika maana unajua mpokeaji ni Mungu na lazima atafungulia madhabahu kuachilia chochote utakachoomba. KWA MAANA HAZINA yako ilipo, ndipo utakapokuwako na moyo wako (MADHABAHU). Mathayo 6;21.
Hili somo linamhusu sana mtu aliyeokoka, KAMA haujaokoka na unatamani ujiunge katika familia ya  Mungu ili upewe uhalali wa KUTAWALA NA KUMILIKI NCHI kwa njia ya Maombi fuatisha sala hii kwa IMANI.
Tafuta MAHALI PA UTULIVU na Sema sala hii pamoja nami kwa Roho na kweli kutoka ndani ya moyo wako;

Bwana Yesu, ninakushukuru kwa Rehema na fadhili zako nyingi ulizozionesha pale ulipojitoa na kufa msalabani kwa ajili yangu mimi mwenye dhambi.Ninakuja kwako, ninaomba unisamehe dhambi zangu zote na unipokee, futa jina langu katika kitabu cha mauti, na uliandike kwenye kitabu cha uzima; unipe uwezo wa kufanyika mtoto  wako tangu sasa. Ninajiachilia kwako, uwe BWANA na mwokozi wa maisha yangu; unitawale katika mwili, nafsi na roho yangu, nikatembee katika mapenzi yako siku zote za maisha yangu.Asante kwa kuwa tangu sasa nimeokoka na kuwa kiumbe kipya. Ya kale yote yamepita na tazama,yamekuwa MAPYA, katika jina lenye NGUVU na MAMLAKA, jina la YESU ninaomba na kuamini kuwa nimepokea sasa.AMEN!!!

Baada ya kusema sala hii amini kuwa upo ndani ya Yesu naye yuko ndani yako. Endelea kuishi katika misingi ya utakatifu katika kujifunza Neno lake na maombi huku ukiufurahia UZURI wa Yesu usiochakaa ndani ya wokovu huu aliokupa.


KISHA FANYA MAOMBI KWA MWONGOZO HUU;-
1.      INGIA KATIKA MAOMBI JUU YA ENEO ULILOPO NA WATU WA ENEO,,

2.      TUBU KWA AJILI YAO NA KWA AJILI YA ENEO AMBALO UMEWEKWA AU UPO IKIWA NI PAMOJA NA UZINZI, RUSHWA, UCHAWI NA USHIRIKINA, UMWAGAJI DAMU ISIYO NA HATIA, UZURUMAJI N.K,,

3.      HARIBU KILA MIFUMO YA KIUTAWALA AMBAYO SHETANI ANAIWEKA KATIKA ARDHI HYO IKIWEMO WACHAWI,WAGANGA, MAPEPO, MAJINI, MIZIMU N.K

4.      RUHUSU MUUNGANIKO (RE-CONNECTION) KATI YA MBINGU (NA KILA KINACHOACHILIWA) NA ARDHI ULIYOPO

5.      KATAA KILA HALI ISIYOKUWA YA UFALME WA MUNGU MAHALI ULIPO KAMA VILE MAGONJWA, VIFO, KUIBIWA, MAJANGA, UMASKINI, KUTESWA NA MAPEPO/ KUFUNGWA, KUTOKUZAA, KUTOKUOLEWA/ KUOA, KUTOPATA KAZI, KUTOFANIKIWA, ARDHI KUZAA MIIBA NA MICHONGOMA N.K

6.      TUMIA DAMU YA YESU NDIYO INAYOKUPA UHALALI WA KUMILIKI KIFALME KATIKA ULIMWENGU WA ROHO MAHALI ULIPO..

WARUMI 8; 31, “ Basi tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo UPANDE WETU ,ni nani aliye JUU YETU?”
MWISHO!!!!
KWA HUDUMA, MAOMBI NA USHAURI ;
www.urejesho. Blogspot.com
Simu no; 0757 35 05 27 au 0717 23 64 90
HUDUMA YA MAOMBI YA UREJESHO

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KURUHUSU UTUKUFU (GLORY) WA BWANA KUFANYA JAMBO KATIKA MAISHA YAKO