NAMNA
 YA
KULILINDA KUSUDI LA MUNGU
 
YAJUE MAMBO YATAKAYO KUSAIDIA KUISHI KWA FAIDA DUNIANI ILI KUJIWEKEA HAZINA NA MAHALI MBINGUNI

NA; MWL. NICKSON KIPANGULA

YALIYOMO
1.                 Shukrani………………………………………………………………………………….3
2.                 Maana Na Umuhimu Wa Kulilinda Kusudi ………………………………..4

3.                 Kubadilishwa Kwa Kusudi Toka Ulimwengu Wa Roho(Sirini) Mpaka Ulimwengu Wa Mwili……………………………………………………………......................11 - 13

4.                 Umuhimu Wa Kuomba Kwa Mzigo ( Maombi Mazito) Yanayokufanya Ulilinde Kusudi Na Kutembea Ndani Yake……………………………13 - 14


5.                 Wafahamu Watu Na Kabila Za Watu Wanaotolewa Punde Unapokuwa Wa Thamani(Kusudi Linatembea/Linaishi) Machoni Pa Mungu………………………………………………………………………………………15

6.                 Nguvu Ifanyayo Kusudi La Mungu Kudhihirika (Kuwa Halisi)………………………………………………………………………………16 - 17

7.                   Mambo Yatakayo Kusaidia Kulilinda Kusudi La Mungu..18 - 19


8.                Mwisho…………………………………………………………………………20


SHUKRANI
Shukrani zimwendee Mungu aliye hai anipaye pumzi ya uhai na bubujiko la kimaandiko kwa ajili ya uponyaji wa watu wake. Nasikia raha, kukutumikia ee Baba katika Kristo Yesu!!
Aidha shukrani ziwaendee wote wanaobeba mzigo kuomba juu ya watumishi waliobeba kusudi la Mungu kuendelea kusambaza habari njema ya Ufalme wa Mungu, Kazi yenu si bure katika Bwana. Mtalipwa kwa wakati.

“Ujumbe huu ukufanye ubadilishe fikra, ufahamu na roho yako kumwelekea Mungu katika jina la Yesu Kristo wa Nazareti, AMEN!!! KARIBU!!!!!!!!!!!”
MAANA NA UMUHIMU WA KULILINDA KUSUDI LA MUNGU

KUSUDI (purpose) – kitu kilichokufanya uwepo ulipo au kuja kuwepo utakapokuwa.
Hakuna kitu kilichopo mahali bila kusudi na hakuna kitu kilichoumbwa pasipo kusudi na pia hata wewe usingekuwepo ulipo bila kusudi. Upo Tanzania,au kwenye mkoa ulipo kwa sababu lipo kusudi Fulani ambalo linatakiwa kutimia tu wewe unapokuwepo pale na bila wewe ni ngumu likatimia.
Lipo jambo ambalo ni maalumu (so specific) linalokufanya uwepo mahali ulipo. Hakuna mwanadamu aliyeachiliwa azaliwe bila kuwepo na kusudi la kuwepo kwake duniani la sivyo, asingezaliwa.
Vipo vitu vingi sana ambavyo wewe unataka uvifanye kwenye maisha yako, pia vipo vitu vingi sana ambavyo Mungu anataka wewe uvifanye kwenye maisha yako, vilevile vipo vitu vingi sana ambavyo shetani anataka wewe uvifanye kwenye maisha yako. Kamwe huwezi kuvifanya vyote. Unafanyaje kujua ni kitu kipi ambacho Mungu anakutaka ukifanye kwenye maisha yako? Au ilimradi kipo kwenye ufahamu wako basi unafanya!!!
Unapotambua wewe ni nani sasa na baadaye na ni kwa kusudi lipi upo utakuwa makini (SERIOUS) – UKIUKOMBOA WAKATI. Maana bidii ya ndani itajengeka na kukufanya uanze kuyaandaa mazingira ya kulitimiza hilo kusudi. Hautakaa kupoteza muda kwa mambo ambayo hayahusiani na kusudi ulilopewa kulitimiza duniani. Watu wengi utasikia anasema ngoja niende kwa rafiki yangu nikapoteze MUDA, haujalijua kusudi wewe!!!
Waefeso 5:10,15-17 biblia inasema, “…mkihakiki ni nini impendezayo Bwana……………….Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; MKIUKOMBOA WAKATI kwa maana zamani hizi ni za UOVU. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.
Tutafakari kidogo hapa;-
1.     Mkihakiki ni nini impendezayo Bwana- hapa anataka tuone kuwa siyo kila kitu utatakiwa kukifanya hata kama una uwezo wa kukifanya na hata kama siyo dhambi kukifanya. KUHAKIKI maana yake ni kujipa uhakika Fulani juu ya jambo Fulani lililoko mbele yako kwa lugha nyingine ni kuamini. Na kuamini kunatokana na Neno la Mungu na pia ukumbuke kuwa Neno la Mungu ndiyo mapenzi ya Mungu. Hii ina maana ya kuwa kitu chochote unachotaka ukifanye ni lazima ukipitishe kwenye Neno la Mungu ili kupata uhakika kama ni mapenzi ya Mungu kukifanya au la.

2.     MKIUKOMBOA WAKATI kwa maana zamani hizi ni za UOVU- Fahamu kuwa huwezi ukakomboa kitu kama hakijatekwa. Hii inamaanisha kuwa kuna kitu ambacho kimeuteka WAKATI ndio maana wakati unahitaji kukombolewa. Kitu hicho ni UOVU. Unapofanya uovu maana yake unapoteza wakati aliokupa Mungu wa kutimiza kusudi alilokupa.Mfano upo kwa rafiki yako mnamsengenya mtu wakati Mungu alikutaka muda huo uwe mahali Fulani unamshuhudia mtu Fulani Neno la Mungu,au upo na mtu kufanya uzinzi na kumbe wakati huo ulipangwa na Mungu uwe mahali Fulani unamuombea mgonjwa Fulani kumnusuru na roho ya mauti inayotaka kummeza ambapo inawezekana wewe ndiye mtu PEKEE wa kumwombea asife. Kumbuka kila sekunde imehesabiwa kwa wewe kufanya jambo Fulani na usipojua kuwa kwa wakati Fulani ulitakiwa kufanya jambo Fulani maana yake utafanya jambo lisilo kwa ule wakati. YOUR TIME IS SO FIXED kiasi kwamba hakuna dakika za majeruhi kama kwenye mpira wa miguu. La sivyo, Mungu aamue mwenyewe kukuongezea muda kwa rehema kama ilivyokuwa kwa mfalme Hezekia (Isaya 38:1 – 6).

 Anamwambia Tengeneza mambo ya nyumba yako MAANA utakufa wala hutapona na hajasema usipotengeneza utakufa. Hii ina maana ya kwamba kutengeneza au kutotengeneza mambo ya nyumba yake hakuathiri kufa kwake ila awaache wakiwa na mwelekeo, maana yake kama ni mirathi,wosia n.k ndio wakati wa kutoa maana punde baada ya huo ugonjwa kinafuata kifo. Na unakuta baada ya kuomba anaambiwa nitaziongeza siku zako kiasi cha miaka kumi na mitano maana yake zilikuwa zimeisha. Hii ni kwa watu wachache sana yaweza kutokea.
Kwa mfano;-
Ukijua kuwa baadaye utakuwa mhubiri wa kimataifa;
1.     Maombi yako mara nyingi yatakuwa kwa kiwango cha kimataifa.maana yake utakuwa unatazama maombi yako kwa kiwango cha kimataifa.
2.     Utakuwa unafanya bidii ya kujua lugha mbalimbali za mataifa mbalimbali.
3.     Utakuwa unafanya mazoezi ya kuhubiri hata ukiwa peke yako au ukiwa na marafiki utakuwa unatamani uwe unawahubiria tu bila kuongea mambo mengine.


Hebu tusome hapa; Marko 11:12-14,20,  Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa. Akaona kwa mbali mtini wenye majani,akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. Akajibu akauambia, tangu leo mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia………………….Na asubuhi walipokuwa wakipita, waliuona ule mti umenyauka toka shinani”.
Sasa hapa tulia kidogo nichimbe;
Anaposema aliona njaa maana yake alihitaji chakula. Na kufuatana na Injili ya Yohana 4:30 – 38, chakula kinachoshibisha njaa ya Yesu ni kuona mapenzi ya Mungu yanatendeka na kazi(kusudi) aliyotumwa na baba yake inatimia.
Sasa twende pamoja;  Anapouangalia mtini anauona umechanua majani ( unachangamka, unasifu na kuabudu,  unatoa sadaka, unafanya maombi hata kufunga,unanena kwa lugha, una imani ya kuhamisha milima n.k) kwa hiyo anatarajia apate kitu kwake, na kumbuka hajasema apate tunda amesema kitu. Kuna aina ya KITU ambacho Yesu anatafuta kwa ule mtini ambacho kinatakiwa kuwepo kwa ule wakati/msimu. Anapousogelea anasema hakuona kitu ila majani. Na nataka uelewe kuwa lile neno “MAANA SI WAKATI WA TINI” Limetamkwa na ule mtini na hii ni katika kujitetea kwa Yesu. Maana tunaambiwa Yesu AKAJIBU akauambia………. Asingeweza kujibu kama hajaulizwa swali nao. Na hii inaonesha haya yalikuwa ni mabishano katika ulimwengu wa roho kati ya ule mti na Yesu. Na inaonesha baada ya ule mtini kuulizwa kuwa mbona umepata neema ya kumwagiliwa maji na kutiwa mbolea hata umekuwa na majani umechanua lakini hutaki kuzaa matunda ninayotaka? Na huo mti ukaongeza swali kwa Yesu kuwa, mbona huu sio wakati wetu akina tini kuzaa matunda? Ndio maana tunaambiwa Yesu akajibu akauambia mtini tangu leo mtu asile matunda kwako. Walipopita asubuhi inayofuata wakakuta umenyauka toka shinani.
Sikiliza, Mungu anapokufanikisha anakupa, kazi, pesa, mke, watoto, nyumba, gari, imani, upako n.k nia yake ni kuona unafanikisha kusudi Fulani ambalo ameliweka ndani yako. Inawezekana hata wewe mpendwa unasema huu sio wakati wangu wa kutumika labda mpaka nimalize shule au nikioa/kuolewa au nikishapata watoto, au nikipata kazi Fulani. Mwingine unasema nitaokoka kwenye mkutano mwingine wa injili kama huu ukija mwakani.
Unapolikubali kusudi la Mungu na kulilinda Mungu anakuheshimu kwa kiwango cha juu sana na kukuona wa thamani. Punda na mwanapunda ambao walitumika na Yesu katika kusudi la kumfikisha Yesu Yerusalemu wasingefunguliwa na wangebaki wamefungwa na pia wasingelitembea juu ya zile nguo watu walizotandika kama wasingelikubali kutumikia lile kusudi. Luka 19:29 – 36. Wapo watu waliuliza mbona mnamfungua mwanapunda? Wakasema, Bwana anamhitaji. Inawezekana ni ndugu zako ndio vizuizi vya wewe kutembea kwenye kusudi la Mungu ama ni wazazi, wanakuzuia kutumika kwa Bwana. Semezana nao katika namna ya maombi waambie Bwana ana haja na mimi niachieni nimtumikie katika jina la Yesu. Lazima tu watakuachilia.
Luka 2:40, “Yule mtoto (YESU) akakua, akaongezeka NGUVU, amejaa HEKIMA, na NEEMA YA MUNGU ilikuwa juu yake”.Hakuna jambo lisilo na mwanzo lazima kuwe na UKUAJI(GROWTH) na KUONGEZEKA(DEVELOPMENT). Huwezi ukaanza tu kufanya semina za kufunga MAHEMA au huduma za nchi za nje wakati kuweza kuhubiria hata watu kumi huwezi bado. Au unategemea uwe daktari bingwa wa upasuaji wakati hata kupasua vyura au mende inakushinda. Au eti uwe waziri wakati hata uenyekiti wa kijiji watu wanakukataa. Lazima ufahamu namna ya kujipanga mwanzo wake. Lazima ukue kimawazo,kifikra na kimtazamo juu ya kusudi ulilopewa ndipo Mungu akupe NGUVU akujaze HEKIMA yake na NEEMA yake ikae juu yako. HEKIMA ni ya msingi kumbuka mwanzo tumesema ili utimize kusudi la Mungu lazima uweze kuukomboa wakati na hauwezi kuukomboa wakati kama haujaenenda kama mtu mwenye HEKIMA.Haleluya!!!!!!!!!!!!!
Yesu katika hali ya kawaida alizaliwa kama mimi na wewe tulivyozaliwa. Ingawa alikuwa Mungu lakini tangu anazaliwa anajua kusudi la Mungu ni nini, kwa hiyo hakuishi kizembe kizembe. Kukua hata kama hupendi utakua tu. Tunaambiwa Yesu akaongezeka NGUVU, HEKIMA na NEEMA YA MUNGU. Vitu hivi haviji tu lazima kuna bidii inayohitajika ndani yako ambayo inakufanya upate hiyo HEKIMA. HEKIMA ni kuwa na uwezo wa kupambanua mambo ili kujua lipi ni sahihi na lipi siyo sahihi. Na Hekima ni juu ( BEYOND ) ya  AKILI / UELEWA wa mwanadamu. Na ndiyo maana mtu anaweza akawa na akili sana au amesoma sana lakini akakosa HEKIMA.
Kwani hujaona wewe, madaktari ambao wanajua kabisa kuwa pombe na sigara vina madhara makubwa mno kwa afya ya binadamu, ikiwemo mapafu, maini, figo, mishipa ya damu,kisukari, vidonda vya tumbo n.k lakini ni watumiaji kupindukia??? HEKIMA iko wapi???? Wana akili lakini wamekosa hekima.
Kuna process (mchakato ) ambao Yesu alikuwa akifanya katika ulimwengu wa roho kutafuta HEKIMA ya Mungu. Hekima inatafutwa kwa bidii. Mithali 8:12,17.  Yesu alikuwa na kuongezeka kwa sababu alikuwa anajua hapa lazima nifikie KIWANGO Fulani cha HEKIMA, NGUVU na NEEMA YA MUNGU ili niweze kutimiza KUSUDI la Mungu aliloniwekea duniani.
Yesu angekosa Hekima na Neema ya Mungu yamkini angeweza kufanya akamatwe mapema hata kabla hajawaandaa watu kabla ya kufa kwake. Angekosa NGUVU ya kiwango Fulani inawezekana angeshindwa kuyabeba MATESO ambayo yalikuwa juu yake.
Elewa kitu hiki; ukiondoa Mungu, kila kitu kina mwanzo wake. Watu husema , “Mbuyu nao ulianza kama mchicha”.
Hebu turejee kitabu cha Yohana 1;1-3 nayo inasema, “ Hapo mwanzo kulikuwapo na NENO naye NENO alikuwapo kwa Mungu, naye NENO alikuwa ni Mungu. Huyo(NENO) mwanzo alikuwa kwa Mungu, vyote vilifanyika kwa huyo(NENO) wala pasipo yeye (NENO) hakukufanyika chochote kilichofanyika”.
Hapa napenda uelewe kitu hiki; anaposema hapo mwanzo ina maanisha ni mwanzo wa kitu Fulani. Na anataka kutueleza kuwa kuna aliyekuwepo kwenye huo mwanzo wa hicho kitu Fulani ili kufanya kitu Fulani kitokee na pasipo yeye kisingewezekana kutokea. NENO ndiye aliyekuwepo kwenye hiyo mwanzo na ndiye aliyefanya vitu vyote kufanyika kwa yeye ( vinavyoonekana na visivyoonekana). Kwa Mujibu wa Yohana 1;14,ambapo inasema,  “Naye NENO akafanyika mwili, akakaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake. Utukufu kama wa mwana wa pekee atokaye kwa baba, amejaa neema na kweli” ni dhahiri kuwa anazungumza kwa habari za NENO kama YESU.
Labda tuangalie kidogo mfumo wa uumbaji ambao Mungu alitumia kuumba vitu vyote kama unavyojionesha katika kitabu hiki cha Mwanzo 1; 1-3 ambapo inasema, “ Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na nchi, nayo nchi ilikuwa ukiwa tena utupu. Roho ya Mungu ikatulia kwenye vilindi vya uso wa maji. Mungu akasema(NENO), na iwe nuru ikawa nuru.Mungu akaona ya kuwa nuru ni njema. Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja”.
Sasa hapa anaposema “……Roho ya Mungu ikatulia juu ya vilindi vya uso wa maji…….” ana maana kuwa Roho anasubiri ushirika Fulani. Na ndiyo maana tunaona Mungu Baba akimwachilia NENO(YESU) kumruhusu Roho mtakatifu kuambatana naye ili kwenda kufanya Nuru iwepo.
Watu wengi huwa wakifikiri juu ya makusudi kwenye maisha yao wanakata tamaa hususani wanapowazo namna wani wataweza kulifikia kusudi na kutembea ndani yake. Lakini hapo tunaona wazi kuwa Roho mtakatifu hutulia kilindini pa uso wa maji( mahali pa utulivu ) ili kusubiri kusikia sauti ya Mungu( NENO ) ili atende kile NENO anasema ama kutoa mwongozo.
Ili Roho Mtakatifu ayatendee kazi maombi yako ni lazima yaambatane na NENO na si kelele maana ana maana nzuri tu kukaa kwenye vilindi vya uso wa maji anatafuta utulivu. KELELE tafsiri yake ni maombi ya mwenye dhambi.
BIBLIA inasema, “Maombi ya mwenye dhambi ni kelele mbele za Mungu..” Maana yake ni kwamba unapomuendea Mungu kwa lengo la kupeleka maombi mbele zake sharti ujue Roho takatifu hatavumilia maombi yasiyoambatana na Toba ikiwa mwombaji haujajitakasa.
Pia ufahamu kuwa Roho mtakatifu hatii maombi ilimradi yameombwa na mtakatifu ila anatii tu maombi ambayo yamebebwa na NENO ndani yake( Holy Spirit doesn’t respond to any prayers BUT he only respond to the prayers contented with The WORD OF GOD). Ndiyo maana hata Yesu anawaambia wanafunzi wake katika Yohana 6; 24, “……Hata sasa hamjaomba NENO lolote kwa jina langu. Ombeni, nanyi mtapewa ili furaha yangu iwe timilifu”. Utashangaa ni kwanini anawaambia hawajaomba wakati kila mara anapanda nao mlimani kuomba?? Jibu ni hili, Yesu anawaambia hawajaomba NENO, inawezekana wameomba maombi mengi sana lakini hayajabeba NENO ndani yake.
Haiyamkini, hata wewe umekuwa ukiomba sana mipango yako maishani ipate kutimia na umekuwa ukimlilia Mungu muda mwingi lakini huoni matokeo au udhihirisho wa maombi yako. Fahamu kuwa NENO LA MUNGU ndiyo MAPENZI YA MUNGU na ndiyo MAKUSUDI YA MUNGU. Lazima maombi yako yajae kwenye mpango wa Mungu,  au makusudi ya Mungu la sivyo utabaki kusema mbona Mungu unasema maandalio ya moyo ni ya mwanadamu??? Lakini anasema bali jawabu la ulimi( NENO ) linatoka kwa Mungu. Jizoeze kupitisha kwenye NENO la Mungu jambo lolote kabla hujaliomba. Na biblia inasema kila NENO la Mungu limehakikishwa,yeye ni ngao yake amwaminiye.
Kumbuka; Sababu ya wanafunzi kutomwacha Yesu kabla hawajajua kuwa ni Mungu ni kwa sababu ya NENO lake. Yohana 6;66-69, “…….Basi Yesu akawaambia wale Tenashara, Je, na ninyi mwataka kuondoka? Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani(mwingine)? Wewe unayo MANENO ya UZIMA WA MILELE……”



KUBADILISHWA KWA KUSUDI TOKA ULIMWENGU WA ROHO(SIRINI) MPAKA ULIMWENGU WA MWILI
Ili kulifahamu kusudi na kutembea ndani ya hilo kusudi lazima uingie katika ulimwengu wa roho ili ufahamu ni nini ambacho kipo kwa ajili yako au wewe upo kwa ajili ya nini katika ulimwengu wa dunia hii. La sivyo unaweza ukaishi nje ya kusudi au ukafa kabla ya wakati wako kwa sababu Mungu hawezi kukuvumilia wewe ambaye unaishi bila kuwa ndani ya kusudi.  Kila tawi ndani yangu lisilozaa (matunda) huliondoa, na kila tawi lizaalo hulisafisha ili lizidi kuzaa”.Yohana 15;2
Wapo malaika ambao wanatembea na wewe siku zote ndio ambao wana kutathmini( evaluate) mambo unayoyafanya kama yapo ndani ya kusudi au la. Halafu wanapeleka ujumbe kwa Mungu kuwa huyu mtu ni kweli yupo duniani anaishi,anakula, anafanya kazi n.k lakini hata sasa miaka 10,15,30 au zaidi aliyo nayo bado yupo nje ya kusudi lako.
Fikiria, kama wewe unataka kujenga nyumba ya ghorofa mbili kwa mwaka mmoja na umewatafuta mafundi ambao unajua watakujengea, na ukawapa vifaa vyote vya ujenzi badala yake baada ya miezi nane unapokagua maendeleo ya jingo ukakuta wamejenga kijumba chenye chumba kimoja au wameshikilia tu fedha na vifaa vya ujenzi wala hawana habari, utawafanya nini?
Yeremia 1:11-12 inasema, “ Tena neno la BWANA likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema naona ufito wa mlozi. Ndipo BWANA akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neon langu, ili nilitimize”. Baada ya Yeremia kuona ufito wa mlozi NDIPO Bwana anamwambia umeona VEMA, maana ninaliangalia Neno langu ili nilitimize maana yake asingeona vema asingejua kama Mungu analiangalia Neno lake( neno lililobebwa ndani ya tafsiri ya UFITO WA MLOZI).
Ilimpasa Yeremia aingie katika ulimwengu wa KIMAONO ili aweze;-
1.    Kuona kile Mungu anamwonesha (UFITO WA MLOZI)
2.    Kujua tafsiri yake (HUO UFITO WA MLOZI UNAVYOMAANISHA)
KUMBUKA; Pasipo MAONO watu huacha kujizuia(wanaangamia) Mithali 29;18-19.
When you live with VISION;- You will not go ANYWHERE but you will go to the SPECIFIC SOMEWHERE, You will not live with ANYONE but you will live with the SPECIFIC SOME ONE, you will not do ANYTHING but you will do the SPECIFIC SOMETHING, because what you SEE is what you are DOING..Haleluyaaaa…..!!!!!!!!!!
Isaya 45;3, “….nami nitakupa wewe hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli ….”
USIPOONA VEMA  ni tatizo maana KUSUDI linaendelea kujificha. Hii ni KANUNI ya kiroho. Ndio maana anasema hapa “….HAZINA ZA GIZANI….” [ Zimefichwa sirini ili NONDO  na KUTU visiweze kuharibu]. Ndio maana katika Mathayo6;19-21 unaambiwa Jiwekeeni HAZINA Mbinguni [ NONDO, KUTU, wala WEVI hawaibi ]. ANAKUTUNZIA MAHALI PA USALAMA maana yake bila kuwa na MACHO YA ROHONI utakufa na hazina ziko palepale zilipohifadhiwa. Baada ya hapo watapewa watu wengine.
Sambamba na neno la Warumi 12;2, “Wala msiifuatishe NAMNA(JINSI AU MFUMO-STYLE) ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya NIA[ MAKUSUDI/MAWAZO YA KIMAAMUZI] zenu, mpate kujua HAKIKA MAPENZI[ MAKUSUDI ] ya Mungu yaliyo MEMA, ya kumpendeza, na UKAMILIFU”. Tunajifunza kuwa; kutofuatisha NAMNA ya Dunia hii kunafanya NIA [MAKUSUDI] yako yageuzwe upya naweupate kuyajua na kuendana na MAPENZI[MAKUSUDI] ya Mungu. Namna ya dunia katika; kunena, kutenda, kuvaa, kula na kunywa, namna ya kutatua matatizo n.k.


UMUHIMU WA KUOMBA KWA MZIGO ( MAOMBI MAZITO) YANAYOKUFANYA ULILINDE KUSUDI NA KUTEMBEA NDANI YAKE
1.    MAOMBI YA YESU( 3 times in 3 hours)
-         Haya maombi yalikuwa mazito kiasi cha kuachilia DAMU (UHAI) juu ya kile alichokuwa anakitafuta (KUSUDI) kwa yeye kuwepo duniani la sivyo ANGELIPOTEZA KUSUDI. Luka 22;40-46.( Aliwaambia KESHENI msije mkaingia MAJARIBUNI)
TAMBUA; moja ya sababu za shetani kuachilia  MAJARIBU (VISHAWISHI) ni KUKUTOA KWENYE KUSUDI ULILOLIBEBA.
i.                   MFANO WA KWANZA; Isaka katika Mwanzo 25;29-34
ii.                MFANO WA PILI; Yesu katika Luka 4;1- 4.
Katika mifano hii yote tunaona shetani akiwajaribu kwa chakula katika kutaka kuwafanya wapoteze KUSUDI walilopewa na Mungu. Watu wengi hutoka kwenye kusudi la Mungu kwa sababu tu ya chakula (hawataki maombi ya kufunga).
Lipo AGANO ambalo Mungu anataka alitimize kupitia wewe kuwapo mahali Fulani. Usipokuwepo unakuwa unavuruga KUSUDI/RATIBA. Danieli 10;1 – 3,13, Danieli 9;1 – 27. Danieli baada ya kugundua kusudi la Mungu kumweka pamoja na watu wake kule Babeli Anazama kwenye maombi mazito pasipo kujali uwepo wa nyama nzuri wala chakula kitamu. Na kwa sababu anajua umuhimu wa lile jambo anang’ang’ana mpaka pale Mungu anapojifunua kwake kupitia malaika.
Kuna mambo mengine yamkini unafanya uzembe katika kuomba ni kwa sababu haujajua umuhimu wake kwako na kwa Mungu, laiti ungejua umuhimu wake, hata radha ya chakula usingeikumbuka.




WAFAHAMU WATU NA KABILA ZA WATU WANAOTOLEWA PUNDE UNAPOKUWA WA THAMANI(KUSUDI LINATEMBEA/LINAISHI) MACHONI PA MUNGU
Isaya 43;4 biblia inasema, “ Kwa kuwa ulikuwa wa THAMANI  machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, name nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa WATU kwa ajili yako na KABILA ZA WATU kwa ajili ya MAISHA YAKO(MLOLONGO MZIMA WA KULITIMIZA KUSUDI LA MUNGU UKIWA DUNIANI)”. Thamani yako kwa Mungu ni pale ambapo analiona kusudi aliloliweka ndani yako LINAISHI, LINATEMBEA, LINAMLETEA FAIDA. Mungu anakuwa anahangaikia kulipalilia kusudi ndani yako na moja kwa moja (automatically) anakupalilia wewe. Hii ni kwa sababu wewe unakuwa chombo cha thamani ambacho hakivujishi kusudi la Mungu. Kumbuka Kuharibika kwa chombo ndiyo kuharibika kwa kilichobebwa.
Kumbuka nimekwambia Punda aliyekuwa amembeba Yesu Aliweza kufunguliwa(kutolewa utumwa) na kupata heshima Ya kutandikiwa nguo na watu wenye heshima zao kwa sababu alikuwa amelibeba kusudi la Mungu(amembeba Yesu kama MFALME WA AMANI) vinginevyo angebaki hali ileile ya kufungwa. Mathayo 21;1 – 8.
Kwa mujibu wa kitabu cha Isaya 45;1-3 tunaona kuwa Unaposhikilia kusudi la aliyekubebesha kusudi (MUNGU);-
i.       MAPINGO YA CHUMA YANAKATIKA
o   Kila kilichozuia njia yako kuelekea mafanikio kinakatika

ii.    MALANGO YANAFUNGUKA DAIMA
o   Milango katika biashara, elimu, kazi, watoto, mume au mke, kiroho na kiuchumi inafunguka.

iii. ANALEGEZA VIUNO VYA WAFALME
o   Wafalme ni wale wenye mamlaka katika eneo, shule,ofisi,wizara, nchi n.k. utapata upenyo kwao hata kama wengine wanapita kupitia rushwa Mungu aliye mfalme wa wafalme anakupitisha kwao katika jina la Yesu.

Maandiko yanasema katika Mithali 17;8, “Kipawa [KUSUDI] ni kama KITO CHA THAMANI[ MADINI/MINERALS] kwake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa”. KUGEUKA maana yake kufanya kazi iliyokusudiwa na hicho kipawa.




NGUVU IFANYAYO KUSUDI LA MUNGU KUDHIHIRIKA
(KUWA HALISI)
1.    Ni ile inayokuwa IMEHIFADHIWA ndani yako
-         Efeso 3:20, “ Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, KWA KADIRI  ya NGUVU ITENDAYO KAZI NDANI YETU”.

2.    Kiwango cha NGUVU unayohifadhi ndicho kiwango cha juu (maximum) ambacho unaweza kukitoa[ The amount yo DEPOSIT is the amount you CAN DRAW]
-         Isaya 37;3, “ Wakamwambia Hezekia asema hivi, Siku hii ni siku ya dhiki, aibu na matukano; maana watoto (KUSUDI) wa tayari kuzaliwa(KUDHIHIRIKA), wala hapana nguvu za kuwazaa(kufanya kusudi lidhihirike)”.

3.    Lazima kufahamu ni kiwango gani cha NGUVU kinahitajika ili kufanya kusudi kudhihirika
-         Marko 8;22-25, “……………akamwekea mikono yake [kuachilia nguvu] , akamwuliza waona kitu?. Akatazama juu, akasema, naona watu kama miti, inakwenda. NDIPO  akaweka tena mikono yake( anaongeza kuvu kufikia kiwango cha kutimiza kusudi) juu ya macho yake,………..akaona VYOTE WAZIWAZI.

4.    Unapobadilisha KANUNI(FORMULA) umebadilisha MFUMO (SYSTEM) mzima
-         Kanuni ya NGUVU ya Mungu ni kwamba ili iachiliwe lazima jambo inayokwenda kufanya liwe linajenga ufalme wa Mungu au kwa lugha nyingine linatimiza mapenzi ya Mungu.

Yohana 15;16, “……………………..Nami nikawaweka mwende mkazae matunda[ MAKUSUDI YA MUNGU]; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lolote mmwombalo Baba kwa Jina langu awapeni”.
MAMBO YATAKAYO KUSAIDIA KULILINDA KUSUDI LA MUNGU


1. Kuilinda imani
-         Uwe kiroho mara nyingi zaidi ya kuwa kimwili (be more spiritual than social). Roho inatazama zaidi ya jambo[beyond the matter] hii inakusaidia kutambua madhara ya jambo Fulani kiroho juu ya kusudi ulilobeba hata kama kwa nje wewe au watu wengine wanaliona liko vizuri halina shida. Ondoa[Omit ] mambo yote ya kimwili (social) ambayo unayaona kuwa hayana msaada kiroho au yanayoathiri roho yako kiimani.
1Yohana 2;15, “Msiipende dunia wala mambo(mabaya) yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichomo duniani, yaani, tama ya mwili, na tama ya macho, na kiburi cha uzima havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia”.


2.    Fahamu umuhimu wa kujitenga umbali wa kutupa jiwe
Isaya 55;8 – 9, “ Maana MAWAZO yangu (MAKUSUDI) si MAWAZO(MAKUSUDI) yenu, wala NJIA(JINSI YA KUFIKIA KUSUDI) zenu si Njia zangu; asema BWANA……….”
Hapa anatujulisha kuwa ushirika wako na Mungu ndio unaokufanya uwaze kama Mungu awazavyo na upite NJIA ambayo Mungu anataka upite. Hivyo lazima uyajue kuwa kujitenga umbali wa kutupa jiwe kimaombi kunakufanya;-
a.     Usisikie mawazo au maoni ya mwanadamu juu ya maisha yako na kusudi la Mungu juu yako badala yake umsikie Mungu na mawazo yake juu ya kusudi lake ndani yako
b.    Kuongeza umakini na usikivu [CONCENTRATION] wakati Mungu atakapokuwa anasema nawe
c.      Kutafuta WAZO JIPYA (to seek for the NEW IDEA) maana mawazo ya wanadamu ni mengi lakini wazo la Mungu juu ya jambo Fulani ni moja tu.
Yesu alifahamu umuhimu huu ndio maana mara nyingi ilikuwa lazima ajitenge na wanafunzi ili atafute wazo la Mungu la siku. Jizoeshe kila siku kumwambia Mungu kuwa naomba unipe WAZO JIPYA katika maisha yangu, biashara, kazi, elimu, uchumi, kiroho, kifamilia, juu ya ndoa yako, uchumba wako n.k






MWISHO
“ Nakutakia mabadiliko na bidii kuu katika kulitafuta na kulilinda kusudi la Mungu maishani mwako katika jina la Yesu . Usiwe mtu wa hasara hapa duniani,Mungu ajisikie faida ya kukuumba wewe na kukuleta duniani na ufanikiwe katika mambo yote katika jina la Yesu!! AMEEEN…!!!!!!!!!!!!!”

Somo hili limeandaliwa na;-
Mwalimu Nickson Kipangula wa Huduma ya Maombi ya Urejesho.
Kwa maombi na maombezi, maoni na ushauri au kama una swali lolote la Kiroho au kimaisha. Au unataka kuokoka au kurejesha kwa upya uhusiano wako na Mungu. Tumia mawasiliano yafuatayo:-
Simu; 0757 35 05 27
Website; www.urejesho.blogspot.com au www.restorationprayersservice.wordpress.com


NAMNA
 YA
KULILINDA KUSUDI LA MUNGU
 
YAJUE MAMBO YATAKAYO KUSAIDIA KUISHI KWA FAIDA DUNIANI ILI KUJIWEKEA HAZINA NA MAHALI MBINGUNI

NA; MWL. NICKSON KIPANGULA

YALIYOMO
1.                 Shukrani………………………………………………………………………………….3
2.                 Maana Na Umuhimu Wa Kulilinda Kusudi ………………………………..4

3.                 Kubadilishwa Kwa Kusudi Toka Ulimwengu Wa Roho(Sirini) Mpaka Ulimwengu Wa Mwili……………………………………………………………......................11 - 13

4.                 Umuhimu Wa Kuomba Kwa Mzigo ( Maombi Mazito) Yanayokufanya Ulilinde Kusudi Na Kutembea Ndani Yake……………………………13 - 14


5.                 Wafahamu Watu Na Kabila Za Watu Wanaotolewa Punde Unapokuwa Wa Thamani(Kusudi Linatembea/Linaishi) Machoni Pa Mungu………………………………………………………………………………………15

6.                 Nguvu Ifanyayo Kusudi La Mungu Kudhihirika (Kuwa Halisi)………………………………………………………………………………16 - 17

7.                   Mambo Yatakayo Kusaidia Kulilinda Kusudi La Mungu..18 - 19


8.                Mwisho…………………………………………………………………………20


SHUKRANI
Shukrani zimwendee Mungu aliye hai anipaye pumzi ya uhai na bubujiko la kimaandiko kwa ajili ya uponyaji wa watu wake. Nasikia raha, kukutumikia ee Baba katika Kristo Yesu!!
Aidha shukrani ziwaendee wote wanaobeba mzigo kuomba juu ya watumishi waliobeba kusudi la Mungu kuendelea kusambaza habari njema ya Ufalme wa Mungu, Kazi yenu si bure katika Bwana. Mtalipwa kwa wakati.

“Ujumbe huu ukufanye ubadilishe fikra, ufahamu na roho yako kumwelekea Mungu katika jina la Yesu Kristo wa Nazareti, AMEN!!! KARIBU!!!!!!!!!!!”
MAANA NA UMUHIMU WA KULILINDA KUSUDI LA MUNGU

KUSUDI (purpose) – kitu kilichokufanya uwepo ulipo au kuja kuwepo utakapokuwa.
Hakuna kitu kilichopo mahali bila kusudi na hakuna kitu kilichoumbwa pasipo kusudi na pia hata wewe usingekuwepo ulipo bila kusudi. Upo Tanzania,au kwenye mkoa ulipo kwa sababu lipo kusudi Fulani ambalo linatakiwa kutimia tu wewe unapokuwepo pale na bila wewe ni ngumu likatimia.
Lipo jambo ambalo ni maalumu (so specific) linalokufanya uwepo mahali ulipo. Hakuna mwanadamu aliyeachiliwa azaliwe bila kuwepo na kusudi la kuwepo kwake duniani la sivyo, asingezaliwa.
Vipo vitu vingi sana ambavyo wewe unataka uvifanye kwenye maisha yako, pia vipo vitu vingi sana ambavyo Mungu anataka wewe uvifanye kwenye maisha yako, vilevile vipo vitu vingi sana ambavyo shetani anataka wewe uvifanye kwenye maisha yako. Kamwe huwezi kuvifanya vyote. Unafanyaje kujua ni kitu kipi ambacho Mungu anakutaka ukifanye kwenye maisha yako? Au ilimradi kipo kwenye ufahamu wako basi unafanya!!!
Unapotambua wewe ni nani sasa na baadaye na ni kwa kusudi lipi upo utakuwa makini (SERIOUS) – UKIUKOMBOA WAKATI. Maana bidii ya ndani itajengeka na kukufanya uanze kuyaandaa mazingira ya kulitimiza hilo kusudi. Hautakaa kupoteza muda kwa mambo ambayo hayahusiani na kusudi ulilopewa kulitimiza duniani. Watu wengi utasikia anasema ngoja niende kwa rafiki yangu nikapoteze MUDA, haujalijua kusudi wewe!!!
Waefeso 5:10,15-17 biblia inasema, “…mkihakiki ni nini impendezayo Bwana……………….Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; MKIUKOMBOA WAKATI kwa maana zamani hizi ni za UOVU. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.
Tutafakari kidogo hapa;-
1.     Mkihakiki ni nini impendezayo Bwana- hapa anataka tuone kuwa siyo kila kitu utatakiwa kukifanya hata kama una uwezo wa kukifanya na hata kama siyo dhambi kukifanya. KUHAKIKI maana yake ni kujipa uhakika Fulani juu ya jambo Fulani lililoko mbele yako kwa lugha nyingine ni kuamini. Na kuamini kunatokana na Neno la Mungu na pia ukumbuke kuwa Neno la Mungu ndiyo mapenzi ya Mungu. Hii ina maana ya kuwa kitu chochote unachotaka ukifanye ni lazima ukipitishe kwenye Neno la Mungu ili kupata uhakika kama ni mapenzi ya Mungu kukifanya au la.

2.     MKIUKOMBOA WAKATI kwa maana zamani hizi ni za UOVU- Fahamu kuwa huwezi ukakomboa kitu kama hakijatekwa. Hii inamaanisha kuwa kuna kitu ambacho kimeuteka WAKATI ndio maana wakati unahitaji kukombolewa. Kitu hicho ni UOVU. Unapofanya uovu maana yake unapoteza wakati aliokupa Mungu wa kutimiza kusudi alilokupa.Mfano upo kwa rafiki yako mnamsengenya mtu wakati Mungu alikutaka muda huo uwe mahali Fulani unamshuhudia mtu Fulani Neno la Mungu,au upo na mtu kufanya uzinzi na kumbe wakati huo ulipangwa na Mungu uwe mahali Fulani unamuombea mgonjwa Fulani kumnusuru na roho ya mauti inayotaka kummeza ambapo inawezekana wewe ndiye mtu PEKEE wa kumwombea asife. Kumbuka kila sekunde imehesabiwa kwa wewe kufanya jambo Fulani na usipojua kuwa kwa wakati Fulani ulitakiwa kufanya jambo Fulani maana yake utafanya jambo lisilo kwa ule wakati. YOUR TIME IS SO FIXED kiasi kwamba hakuna dakika za majeruhi kama kwenye mpira wa miguu. La sivyo, Mungu aamue mwenyewe kukuongezea muda kwa rehema kama ilivyokuwa kwa mfalme Hezekia (Isaya 38:1 – 6).

 Anamwambia Tengeneza mambo ya nyumba yako MAANA utakufa wala hutapona na hajasema usipotengeneza utakufa. Hii ina maana ya kwamba kutengeneza au kutotengeneza mambo ya nyumba yake hakuathiri kufa kwake ila awaache wakiwa na mwelekeo, maana yake kama ni mirathi,wosia n.k ndio wakati wa kutoa maana punde baada ya huo ugonjwa kinafuata kifo. Na unakuta baada ya kuomba anaambiwa nitaziongeza siku zako kiasi cha miaka kumi na mitano maana yake zilikuwa zimeisha. Hii ni kwa watu wachache sana yaweza kutokea.
Kwa mfano;-
Ukijua kuwa baadaye utakuwa mhubiri wa kimataifa;
1.     Maombi yako mara nyingi yatakuwa kwa kiwango cha kimataifa.maana yake utakuwa unatazama maombi yako kwa kiwango cha kimataifa.
2.     Utakuwa unafanya bidii ya kujua lugha mbalimbali za mataifa mbalimbali.
3.     Utakuwa unafanya mazoezi ya kuhubiri hata ukiwa peke yako au ukiwa na marafiki utakuwa unatamani uwe unawahubiria tu bila kuongea mambo mengine.


Hebu tusome hapa; Marko 11:12-14,20,  Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa. Akaona kwa mbali mtini wenye majani,akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. Akajibu akauambia, tangu leo mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia………………….Na asubuhi walipokuwa wakipita, waliuona ule mti umenyauka toka shinani”.
Sasa hapa tulia kidogo nichimbe;
Anaposema aliona njaa maana yake alihitaji chakula. Na kufuatana na Injili ya Yohana 4:30 – 38, chakula kinachoshibisha njaa ya Yesu ni kuona mapenzi ya Mungu yanatendeka na kazi(kusudi) aliyotumwa na baba yake inatimia.
Sasa twende pamoja;  Anapouangalia mtini anauona umechanua majani ( unachangamka, unasifu na kuabudu,  unatoa sadaka, unafanya maombi hata kufunga,unanena kwa lugha, una imani ya kuhamisha milima n.k) kwa hiyo anatarajia apate kitu kwake, na kumbuka hajasema apate tunda amesema kitu. Kuna aina ya KITU ambacho Yesu anatafuta kwa ule mtini ambacho kinatakiwa kuwepo kwa ule wakati/msimu. Anapousogelea anasema hakuona kitu ila majani. Na nataka uelewe kuwa lile neno “MAANA SI WAKATI WA TINI” Limetamkwa na ule mtini na hii ni katika kujitetea kwa Yesu. Maana tunaambiwa Yesu AKAJIBU akauambia………. Asingeweza kujibu kama hajaulizwa swali nao. Na hii inaonesha haya yalikuwa ni mabishano katika ulimwengu wa roho kati ya ule mti na Yesu. Na inaonesha baada ya ule mtini kuulizwa kuwa mbona umepata neema ya kumwagiliwa maji na kutiwa mbolea hata umekuwa na majani umechanua lakini hutaki kuzaa matunda ninayotaka? Na huo mti ukaongeza swali kwa Yesu kuwa, mbona huu sio wakati wetu akina tini kuzaa matunda? Ndio maana tunaambiwa Yesu akajibu akauambia mtini tangu leo mtu asile matunda kwako. Walipopita asubuhi inayofuata wakakuta umenyauka toka shinani.
Sikiliza, Mungu anapokufanikisha anakupa, kazi, pesa, mke, watoto, nyumba, gari, imani, upako n.k nia yake ni kuona unafanikisha kusudi Fulani ambalo ameliweka ndani yako. Inawezekana hata wewe mpendwa unasema huu sio wakati wangu wa kutumika labda mpaka nimalize shule au nikioa/kuolewa au nikishapata watoto, au nikipata kazi Fulani. Mwingine unasema nitaokoka kwenye mkutano mwingine wa injili kama huu ukija mwakani.
Unapolikubali kusudi la Mungu na kulilinda Mungu anakuheshimu kwa kiwango cha juu sana na kukuona wa thamani. Punda na mwanapunda ambao walitumika na Yesu katika kusudi la kumfikisha Yesu Yerusalemu wasingefunguliwa na wangebaki wamefungwa na pia wasingelitembea juu ya zile nguo watu walizotandika kama wasingelikubali kutumikia lile kusudi. Luka 19:29 – 36. Wapo watu waliuliza mbona mnamfungua mwanapunda? Wakasema, Bwana anamhitaji. Inawezekana ni ndugu zako ndio vizuizi vya wewe kutembea kwenye kusudi la Mungu ama ni wazazi, wanakuzuia kutumika kwa Bwana. Semezana nao katika namna ya maombi waambie Bwana ana haja na mimi niachieni nimtumikie katika jina la Yesu. Lazima tu watakuachilia.
Luka 2:40, “Yule mtoto (YESU) akakua, akaongezeka NGUVU, amejaa HEKIMA, na NEEMA YA MUNGU ilikuwa juu yake”.Hakuna jambo lisilo na mwanzo lazima kuwe na UKUAJI(GROWTH) na KUONGEZEKA(DEVELOPMENT). Huwezi ukaanza tu kufanya semina za kufunga MAHEMA au huduma za nchi za nje wakati kuweza kuhubiria hata watu kumi huwezi bado. Au unategemea uwe daktari bingwa wa upasuaji wakati hata kupasua vyura au mende inakushinda. Au eti uwe waziri wakati hata uenyekiti wa kijiji watu wanakukataa. Lazima ufahamu namna ya kujipanga mwanzo wake. Lazima ukue kimawazo,kifikra na kimtazamo juu ya kusudi ulilopewa ndipo Mungu akupe NGUVU akujaze HEKIMA yake na NEEMA yake ikae juu yako. HEKIMA ni ya msingi kumbuka mwanzo tumesema ili utimize kusudi la Mungu lazima uweze kuukomboa wakati na hauwezi kuukomboa wakati kama haujaenenda kama mtu mwenye HEKIMA.Haleluya!!!!!!!!!!!!!
Yesu katika hali ya kawaida alizaliwa kama mimi na wewe tulivyozaliwa. Ingawa alikuwa Mungu lakini tangu anazaliwa anajua kusudi la Mungu ni nini, kwa hiyo hakuishi kizembe kizembe. Kukua hata kama hupendi utakua tu. Tunaambiwa Yesu akaongezeka NGUVU, HEKIMA na NEEMA YA MUNGU. Vitu hivi haviji tu lazima kuna bidii inayohitajika ndani yako ambayo inakufanya upate hiyo HEKIMA. HEKIMA ni kuwa na uwezo wa kupambanua mambo ili kujua lipi ni sahihi na lipi siyo sahihi. Na Hekima ni juu ( BEYOND ) ya  AKILI / UELEWA wa mwanadamu. Na ndiyo maana mtu anaweza akawa na akili sana au amesoma sana lakini akakosa HEKIMA.
Kwani hujaona wewe, madaktari ambao wanajua kabisa kuwa pombe na sigara vina madhara makubwa mno kwa afya ya binadamu, ikiwemo mapafu, maini, figo, mishipa ya damu,kisukari, vidonda vya tumbo n.k lakini ni watumiaji kupindukia??? HEKIMA iko wapi???? Wana akili lakini wamekosa hekima.
Kuna process (mchakato ) ambao Yesu alikuwa akifanya katika ulimwengu wa roho kutafuta HEKIMA ya Mungu. Hekima inatafutwa kwa bidii. Mithali 8:12,17.  Yesu alikuwa na kuongezeka kwa sababu alikuwa anajua hapa lazima nifikie KIWANGO Fulani cha HEKIMA, NGUVU na NEEMA YA MUNGU ili niweze kutimiza KUSUDI la Mungu aliloniwekea duniani.
Yesu angekosa Hekima na Neema ya Mungu yamkini angeweza kufanya akamatwe mapema hata kabla hajawaandaa watu kabla ya kufa kwake. Angekosa NGUVU ya kiwango Fulani inawezekana angeshindwa kuyabeba MATESO ambayo yalikuwa juu yake.
Elewa kitu hiki; ukiondoa Mungu, kila kitu kina mwanzo wake. Watu husema , “Mbuyu nao ulianza kama mchicha”.
Hebu turejee kitabu cha Yohana 1;1-3 nayo inasema, “ Hapo mwanzo kulikuwapo na NENO naye NENO alikuwapo kwa Mungu, naye NENO alikuwa ni Mungu. Huyo(NENO) mwanzo alikuwa kwa Mungu, vyote vilifanyika kwa huyo(NENO) wala pasipo yeye (NENO) hakukufanyika chochote kilichofanyika”.
Hapa napenda uelewe kitu hiki; anaposema hapo mwanzo ina maanisha ni mwanzo wa kitu Fulani. Na anataka kutueleza kuwa kuna aliyekuwepo kwenye huo mwanzo wa hicho kitu Fulani ili kufanya kitu Fulani kitokee na pasipo yeye kisingewezekana kutokea. NENO ndiye aliyekuwepo kwenye hiyo mwanzo na ndiye aliyefanya vitu vyote kufanyika kwa yeye ( vinavyoonekana na visivyoonekana). Kwa Mujibu wa Yohana 1;14,ambapo inasema,  “Naye NENO akafanyika mwili, akakaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake. Utukufu kama wa mwana wa pekee atokaye kwa baba, amejaa neema na kweli” ni dhahiri kuwa anazungumza kwa habari za NENO kama YESU.
Labda tuangalie kidogo mfumo wa uumbaji ambao Mungu alitumia kuumba vitu vyote kama unavyojionesha katika kitabu hiki cha Mwanzo 1; 1-3 ambapo inasema, “ Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na nchi, nayo nchi ilikuwa ukiwa tena utupu. Roho ya Mungu ikatulia kwenye vilindi vya uso wa maji. Mungu akasema(NENO), na iwe nuru ikawa nuru.Mungu akaona ya kuwa nuru ni njema. Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja”.
Sasa hapa anaposema “……Roho ya Mungu ikatulia juu ya vilindi vya uso wa maji…….” ana maana kuwa Roho anasubiri ushirika Fulani. Na ndiyo maana tunaona Mungu Baba akimwachilia NENO(YESU) kumruhusu Roho mtakatifu kuambatana naye ili kwenda kufanya Nuru iwepo.
Watu wengi huwa wakifikiri juu ya makusudi kwenye maisha yao wanakata tamaa hususani wanapowazo namna wani wataweza kulifikia kusudi na kutembea ndani yake. Lakini hapo tunaona wazi kuwa Roho mtakatifu hutulia kilindini pa uso wa maji( mahali pa utulivu ) ili kusubiri kusikia sauti ya Mungu( NENO ) ili atende kile NENO anasema ama kutoa mwongozo.
Ili Roho Mtakatifu ayatendee kazi maombi yako ni lazima yaambatane na NENO na si kelele maana ana maana nzuri tu kukaa kwenye vilindi vya uso wa maji anatafuta utulivu. KELELE tafsiri yake ni maombi ya mwenye dhambi.
BIBLIA inasema, “Maombi ya mwenye dhambi ni kelele mbele za Mungu..” Maana yake ni kwamba unapomuendea Mungu kwa lengo la kupeleka maombi mbele zake sharti ujue Roho takatifu hatavumilia maombi yasiyoambatana na Toba ikiwa mwombaji haujajitakasa.
Pia ufahamu kuwa Roho mtakatifu hatii maombi ilimradi yameombwa na mtakatifu ila anatii tu maombi ambayo yamebebwa na NENO ndani yake( Holy Spirit doesn’t respond to any prayers BUT he only respond to the prayers contented with The WORD OF GOD). Ndiyo maana hata Yesu anawaambia wanafunzi wake katika Yohana 6; 24, “……Hata sasa hamjaomba NENO lolote kwa jina langu. Ombeni, nanyi mtapewa ili furaha yangu iwe timilifu”. Utashangaa ni kwanini anawaambia hawajaomba wakati kila mara anapanda nao mlimani kuomba?? Jibu ni hili, Yesu anawaambia hawajaomba NENO, inawezekana wameomba maombi mengi sana lakini hayajabeba NENO ndani yake.
Haiyamkini, hata wewe umekuwa ukiomba sana mipango yako maishani ipate kutimia na umekuwa ukimlilia Mungu muda mwingi lakini huoni matokeo au udhihirisho wa maombi yako. Fahamu kuwa NENO LA MUNGU ndiyo MAPENZI YA MUNGU na ndiyo MAKUSUDI YA MUNGU. Lazima maombi yako yajae kwenye mpango wa Mungu,  au makusudi ya Mungu la sivyo utabaki kusema mbona Mungu unasema maandalio ya moyo ni ya mwanadamu??? Lakini anasema bali jawabu la ulimi( NENO ) linatoka kwa Mungu. Jizoeze kupitisha kwenye NENO la Mungu jambo lolote kabla hujaliomba. Na biblia inasema kila NENO la Mungu limehakikishwa,yeye ni ngao yake amwaminiye.
Kumbuka; Sababu ya wanafunzi kutomwacha Yesu kabla hawajajua kuwa ni Mungu ni kwa sababu ya NENO lake. Yohana 6;66-69, “…….Basi Yesu akawaambia wale Tenashara, Je, na ninyi mwataka kuondoka? Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani(mwingine)? Wewe unayo MANENO ya UZIMA WA MILELE……”



KUBADILISHWA KWA KUSUDI TOKA ULIMWENGU WA ROHO(SIRINI) MPAKA ULIMWENGU WA MWILI
Ili kulifahamu kusudi na kutembea ndani ya hilo kusudi lazima uingie katika ulimwengu wa roho ili ufahamu ni nini ambacho kipo kwa ajili yako au wewe upo kwa ajili ya nini katika ulimwengu wa dunia hii. La sivyo unaweza ukaishi nje ya kusudi au ukafa kabla ya wakati wako kwa sababu Mungu hawezi kukuvumilia wewe ambaye unaishi bila kuwa ndani ya kusudi.  Kila tawi ndani yangu lisilozaa (matunda) huliondoa, na kila tawi lizaalo hulisafisha ili lizidi kuzaa”.Yohana 15;2
Wapo malaika ambao wanatembea na wewe siku zote ndio ambao wana kutathmini( evaluate) mambo unayoyafanya kama yapo ndani ya kusudi au la. Halafu wanapeleka ujumbe kwa Mungu kuwa huyu mtu ni kweli yupo duniani anaishi,anakula, anafanya kazi n.k lakini hata sasa miaka 10,15,30 au zaidi aliyo nayo bado yupo nje ya kusudi lako.
Fikiria, kama wewe unataka kujenga nyumba ya ghorofa mbili kwa mwaka mmoja na umewatafuta mafundi ambao unajua watakujengea, na ukawapa vifaa vyote vya ujenzi badala yake baada ya miezi nane unapokagua maendeleo ya jingo ukakuta wamejenga kijumba chenye chumba kimoja au wameshikilia tu fedha na vifaa vya ujenzi wala hawana habari, utawafanya nini?
Yeremia 1:11-12 inasema, “ Tena neno la BWANA likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema naona ufito wa mlozi. Ndipo BWANA akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neon langu, ili nilitimize”. Baada ya Yeremia kuona ufito wa mlozi NDIPO Bwana anamwambia umeona VEMA, maana ninaliangalia Neno langu ili nilitimize maana yake asingeona vema asingejua kama Mungu analiangalia Neno lake( neno lililobebwa ndani ya tafsiri ya UFITO WA MLOZI).
Ilimpasa Yeremia aingie katika ulimwengu wa KIMAONO ili aweze;-
1.    Kuona kile Mungu anamwonesha (UFITO WA MLOZI)
2.    Kujua tafsiri yake (HUO UFITO WA MLOZI UNAVYOMAANISHA)
KUMBUKA; Pasipo MAONO watu huacha kujizuia(wanaangamia) Mithali 29;18-19.
When you live with VISION;- You will not go ANYWHERE but you will go to the SPECIFIC SOMEWHERE, You will not live with ANYONE but you will live with the SPECIFIC SOME ONE, you will not do ANYTHING but you will do the SPECIFIC SOMETHING, because what you SEE is what you are DOING..Haleluyaaaa…..!!!!!!!!!!
Isaya 45;3, “….nami nitakupa wewe hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli ….”
USIPOONA VEMA  ni tatizo maana KUSUDI linaendelea kujificha. Hii ni KANUNI ya kiroho. Ndio maana anasema hapa “….HAZINA ZA GIZANI….” [ Zimefichwa sirini ili NONDO  na KUTU visiweze kuharibu]. Ndio maana katika Mathayo6;19-21 unaambiwa Jiwekeeni HAZINA Mbinguni [ NONDO, KUTU, wala WEVI hawaibi ]. ANAKUTUNZIA MAHALI PA USALAMA maana yake bila kuwa na MACHO YA ROHONI utakufa na hazina ziko palepale zilipohifadhiwa. Baada ya hapo watapewa watu wengine.
Sambamba na neno la Warumi 12;2, “Wala msiifuatishe NAMNA(JINSI AU MFUMO-STYLE) ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya NIA[ MAKUSUDI/MAWAZO YA KIMAAMUZI] zenu, mpate kujua HAKIKA MAPENZI[ MAKUSUDI ] ya Mungu yaliyo MEMA, ya kumpendeza, na UKAMILIFU”. Tunajifunza kuwa; kutofuatisha NAMNA ya Dunia hii kunafanya NIA [MAKUSUDI] yako yageuzwe upya naweupate kuyajua na kuendana na MAPENZI[MAKUSUDI] ya Mungu. Namna ya dunia katika; kunena, kutenda, kuvaa, kula na kunywa, namna ya kutatua matatizo n.k.


UMUHIMU WA KUOMBA KWA MZIGO ( MAOMBI MAZITO) YANAYOKUFANYA ULILINDE KUSUDI NA KUTEMBEA NDANI YAKE
1.    MAOMBI YA YESU( 3 times in 3 hours)
-         Haya maombi yalikuwa mazito kiasi cha kuachilia DAMU (UHAI) juu ya kile alichokuwa anakitafuta (KUSUDI) kwa yeye kuwepo duniani la sivyo ANGELIPOTEZA KUSUDI. Luka 22;40-46.( Aliwaambia KESHENI msije mkaingia MAJARIBUNI)
TAMBUA; moja ya sababu za shetani kuachilia  MAJARIBU (VISHAWISHI) ni KUKUTOA KWENYE KUSUDI ULILOLIBEBA.
i.                   MFANO WA KWANZA; Isaka katika Mwanzo 25;29-34
ii.                MFANO WA PILI; Yesu katika Luka 4;1- 4.
Katika mifano hii yote tunaona shetani akiwajaribu kwa chakula katika kutaka kuwafanya wapoteze KUSUDI walilopewa na Mungu. Watu wengi hutoka kwenye kusudi la Mungu kwa sababu tu ya chakula (hawataki maombi ya kufunga).
Lipo AGANO ambalo Mungu anataka alitimize kupitia wewe kuwapo mahali Fulani. Usipokuwepo unakuwa unavuruga KUSUDI/RATIBA. Danieli 10;1 – 3,13, Danieli 9;1 – 27. Danieli baada ya kugundua kusudi la Mungu kumweka pamoja na watu wake kule Babeli Anazama kwenye maombi mazito pasipo kujali uwepo wa nyama nzuri wala chakula kitamu. Na kwa sababu anajua umuhimu wa lile jambo anang’ang’ana mpaka pale Mungu anapojifunua kwake kupitia malaika.
Kuna mambo mengine yamkini unafanya uzembe katika kuomba ni kwa sababu haujajua umuhimu wake kwako na kwa Mungu, laiti ungejua umuhimu wake, hata radha ya chakula usingeikumbuka.




WAFAHAMU WATU NA KABILA ZA WATU WANAOTOLEWA PUNDE UNAPOKUWA WA THAMANI(KUSUDI LINATEMBEA/LINAISHI) MACHONI PA MUNGU
Isaya 43;4 biblia inasema, “ Kwa kuwa ulikuwa wa THAMANI  machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, name nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa WATU kwa ajili yako na KABILA ZA WATU kwa ajili ya MAISHA YAKO(MLOLONGO MZIMA WA KULITIMIZA KUSUDI LA MUNGU UKIWA DUNIANI)”. Thamani yako kwa Mungu ni pale ambapo analiona kusudi aliloliweka ndani yako LINAISHI, LINATEMBEA, LINAMLETEA FAIDA. Mungu anakuwa anahangaikia kulipalilia kusudi ndani yako na moja kwa moja (automatically) anakupalilia wewe. Hii ni kwa sababu wewe unakuwa chombo cha thamani ambacho hakivujishi kusudi la Mungu. Kumbuka Kuharibika kwa chombo ndiyo kuharibika kwa kilichobebwa.
Kumbuka nimekwambia Punda aliyekuwa amembeba Yesu Aliweza kufunguliwa(kutolewa utumwa) na kupata heshima Ya kutandikiwa nguo na watu wenye heshima zao kwa sababu alikuwa amelibeba kusudi la Mungu(amembeba Yesu kama MFALME WA AMANI) vinginevyo angebaki hali ileile ya kufungwa. Mathayo 21;1 – 8.
Kwa mujibu wa kitabu cha Isaya 45;1-3 tunaona kuwa Unaposhikilia kusudi la aliyekubebesha kusudi (MUNGU);-
i.       MAPINGO YA CHUMA YANAKATIKA
o   Kila kilichozuia njia yako kuelekea mafanikio kinakatika

ii.    MALANGO YANAFUNGUKA DAIMA
o   Milango katika biashara, elimu, kazi, watoto, mume au mke, kiroho na kiuchumi inafunguka.

iii. ANALEGEZA VIUNO VYA WAFALME
o   Wafalme ni wale wenye mamlaka katika eneo, shule,ofisi,wizara, nchi n.k. utapata upenyo kwao hata kama wengine wanapita kupitia rushwa Mungu aliye mfalme wa wafalme anakupitisha kwao katika jina la Yesu.

Maandiko yanasema katika Mithali 17;8, “Kipawa [KUSUDI] ni kama KITO CHA THAMANI[ MADINI/MINERALS] kwake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa”. KUGEUKA maana yake kufanya kazi iliyokusudiwa na hicho kipawa.




NGUVU IFANYAYO KUSUDI LA MUNGU KUDHIHIRIKA
(KUWA HALISI)
1.    Ni ile inayokuwa IMEHIFADHIWA ndani yako
-         Efeso 3:20, “ Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, KWA KADIRI  ya NGUVU ITENDAYO KAZI NDANI YETU”.

2.    Kiwango cha NGUVU unayohifadhi ndicho kiwango cha juu (maximum) ambacho unaweza kukitoa[ The amount yo DEPOSIT is the amount you CAN DRAW]
-         Isaya 37;3, “ Wakamwambia Hezekia asema hivi, Siku hii ni siku ya dhiki, aibu na matukano; maana watoto (KUSUDI) wa tayari kuzaliwa(KUDHIHIRIKA), wala hapana nguvu za kuwazaa(kufanya kusudi lidhihirike)”.

3.    Lazima kufahamu ni kiwango gani cha NGUVU kinahitajika ili kufanya kusudi kudhihirika
-         Marko 8;22-25, “……………akamwekea mikono yake [kuachilia nguvu] , akamwuliza waona kitu?. Akatazama juu, akasema, naona watu kama miti, inakwenda. NDIPO  akaweka tena mikono yake( anaongeza kuvu kufikia kiwango cha kutimiza kusudi) juu ya macho yake,………..akaona VYOTE WAZIWAZI.

4.    Unapobadilisha KANUNI(FORMULA) umebadilisha MFUMO (SYSTEM) mzima
-         Kanuni ya NGUVU ya Mungu ni kwamba ili iachiliwe lazima jambo inayokwenda kufanya liwe linajenga ufalme wa Mungu au kwa lugha nyingine linatimiza mapenzi ya Mungu.

Yohana 15;16, “……………………..Nami nikawaweka mwende mkazae matunda[ MAKUSUDI YA MUNGU]; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lolote mmwombalo Baba kwa Jina langu awapeni”.
MAMBO YATAKAYO KUSAIDIA KULILINDA KUSUDI LA MUNGU


1. Kuilinda imani
-         Uwe kiroho mara nyingi zaidi ya kuwa kimwili (be more spiritual than social). Roho inatazama zaidi ya jambo[beyond the matter] hii inakusaidia kutambua madhara ya jambo Fulani kiroho juu ya kusudi ulilobeba hata kama kwa nje wewe au watu wengine wanaliona liko vizuri halina shida. Ondoa[Omit ] mambo yote ya kimwili (social) ambayo unayaona kuwa hayana msaada kiroho au yanayoathiri roho yako kiimani.
1Yohana 2;15, “Msiipende dunia wala mambo(mabaya) yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichomo duniani, yaani, tama ya mwili, na tama ya macho, na kiburi cha uzima havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia”.


2.    Fahamu umuhimu wa kujitenga umbali wa kutupa jiwe
Isaya 55;8 – 9, “ Maana MAWAZO yangu (MAKUSUDI) si MAWAZO(MAKUSUDI) yenu, wala NJIA(JINSI YA KUFIKIA KUSUDI) zenu si Njia zangu; asema BWANA……….”
Hapa anatujulisha kuwa ushirika wako na Mungu ndio unaokufanya uwaze kama Mungu awazavyo na upite NJIA ambayo Mungu anataka upite. Hivyo lazima uyajue kuwa kujitenga umbali wa kutupa jiwe kimaombi kunakufanya;-
a.     Usisikie mawazo au maoni ya mwanadamu juu ya maisha yako na kusudi la Mungu juu yako badala yake umsikie Mungu na mawazo yake juu ya kusudi lake ndani yako
b.    Kuongeza umakini na usikivu [CONCENTRATION] wakati Mungu atakapokuwa anasema nawe
c.      Kutafuta WAZO JIPYA (to seek for the NEW IDEA) maana mawazo ya wanadamu ni mengi lakini wazo la Mungu juu ya jambo Fulani ni moja tu.
Yesu alifahamu umuhimu huu ndio maana mara nyingi ilikuwa lazima ajitenge na wanafunzi ili atafute wazo la Mungu la siku. Jizoeshe kila siku kumwambia Mungu kuwa naomba unipe WAZO JIPYA katika maisha yangu, biashara, kazi, elimu, uchumi, kiroho, kifamilia, juu ya ndoa yako, uchumba wako n.k






MWISHO
“ Nakutakia mabadiliko na bidii kuu katika kulitafuta na kulilinda kusudi la Mungu maishani mwako katika jina la Yesu . Usiwe mtu wa hasara hapa duniani,Mungu ajisikie faida ya kukuumba wewe na kukuleta duniani na ufanikiwe katika mambo yote katika jina la Yesu!! AMEEEN…!!!!!!!!!!!!!”

Somo hili limeandaliwa na;-
Mwalimu Nickson Kipangula wa Huduma ya Maombi ya Urejesho.
Kwa maombi na maombezi, maoni na ushauri au kama una swali lolote la Kiroho au kimaisha. Au unataka kuokoka au kurejesha kwa upya uhusiano wako na Mungu. Tumia mawasiliano yafuatayo:-
Simu; 0757 35 05 27
Website; www.urejesho.blogspot.com au www.restorationprayersservice.wordpress.com

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KURUHUSU UTUKUFU (GLORY) WA BWANA KUFANYA JAMBO KATIKA MAISHA YAKO