TOBA YA KUULETA UFALME WA MUNGU ILI KURUHUSU MAPENZI YA MUNGU YA MBINGUNI YAFANYIKE DUNIANI (sehemu ya 1)

Mathayo 4:17, “ …….tubuni maana ufalme wa Mbinguni umekaribia”.
TOBA – kubadilika mtazamo, fikra, na mwenendo juu ya jambo baya ulilokua unalifanya ( changing mindset and changing lifestyle from bad things to good things).
MWENENDO – Tabia, maneno, mawazo na matendo
Kuna mambo lazima ukubali kuyaacha unapotaka ufalme wa Mungu uingie ndani yako au mahali ulipo ili Mungu atimize alilokusudia katika maisha yako.
Hatuokoki tu kwa sababu tunataka kuingia mbinguni, tunaokoka ili tuunganishwe na nguvu ya Mungu ya kutulinda na Yule mwovu tukiwa tungali duniani.
MAMBO AMBAYO MUNGU ANATULINDA TUKIWA NA UFALME WAKE
Kazi ya shetani ni kuiba, kuchinja na kuharibu Makusudi/mipango ya Mungu ndani yetu.
Kumbuka: Ili Mungu afanye jambo Fulani kwako ni lazima akushirikishe.
Warumi 8:28, “ Nasi twajua kuwa katika MAMBO YOTE Mungu hufanya kazi pamoja na wampendao katika kuwapatia mema”.
Kwanza, anaanza kuingiza WAZO ndani yako litakalofanya mawazo yasiyofaa ndani  yako yaondoke. Isaya 55:8. Baada ya hapo ndipo husema, “…NA TUFANYE….( gari, nyumba, ndoa nzuri, viongozi waadilifu, mtoto, mume/mke n.k”) vitakavyo fanya huyu mtu awe na uwezo wa kuuendeleza ufalme wangu duniani kwa kuzaa matunda.
Kuna toba ya kukufanya uokoke maana yake upate kibali cha kuingia Mbinguni. Hii inamhusu mtu binafsi
Kuna toba iletayo ufalme wa Mungu duniani. Hii inamhusu mtu anayetubu, ardhi, anga na watu wa ardhi katika eneo husika. Unapotubu  kwa ajili ya ardhi ya eneo kwa mambo mabaya yanayofanyika “baa, uzinzi, uchawi, ushirikina n.k” uwe na uhakika lazima mwana wa Mungu( Yesu ) anadhihirika, hii ni kutokana na kuwa ufalme wa Mungu umeshuka mahali hapo. Yesu anakuwepo kwa kazi kuu moja “AZIVUNJE KAZI ZA IBILISI”. 1Yohana 3:8b.
Ili uwe ndani ya ufalme wa Mungu lazima ubadili mfumo wa maisha yako. Usiishi tena kama MTUMWA, ishi kama MFALME. Automatically utajikuta unaacha kusema, “shetani kajiinua” au “shetani alinipitia”.
UTUMWA ni kufanya kitu ambacho haupendi kukifanya au kutoweza kufanya kitu ambacho ulikuwa unapenda ukifanye. Wapendwa wengi leo hawapendi kuonekana Malaya, wahuni, machangudoa, watu wa vijiweni n.k Lakini unapoangalia mavazi yao ( vijisuruali kwa wadada, vinguo vinavyoonesha maungo yao, mapambo na misuko ya kikahaba, kurembua kimahaba, tattoo na pete zisizo na tafsiri [hayupo kwenye uchumba wala ndoa], milegezo wakaka, mizaha na lugha za kihuni) utajua kuwa wanatumikishwa na UFALME WA SHETANI. Aidha, wasingependa pia kuugua, kuhuzunishwa, kupoteza wapendwa wao kishirikina, kupata ajali n.k. Vilevile wapendwa wengi leo wangependa wawe wameshaoa/kuolewa, wana kazi, wanafaulu masomo, wana mtoto, biashara zinafanikiwa, wana nyumba, kiwanja, n.k. Lakini mpaka leo hawaoni uhalisia wa hayo yote. Shida nini??? UTUMWA!!!!
Biblia inasema, “…………wala mtumwa hakai NYUMBANI siku zote; mwana hukaa nyumbani siku zote. Basi MWANA akiwaweka huru mtakuwa huru kwelikweli”. Yohana 8;31-36.
Kumbuka: hapa anazungumza na Wayahudi ambao tayari wamesha mwamini. Kwa leo tungesema ambao WAMEOKOKA, tunakwenda sawa???
Sasa nisikilize:- Anaposema mtumwa hakai nyumbani siku zote maana yake kuna wakati una tamani ukae katika utakatifu, udumu katika mafanikio uliyonayo, usipatwe na matatizo kutoka ufalme wa giza, ufaulu siku zote, ukae na ndoa inayodumu siku zote, uwe na uchumba wa kudumu kukupeleka kwenye ndoa , lakini hauwezi inashindikana. Shida nini?????? “ MTUMWA HAKAI NYUMBANI SIKU ZOTE” kumbuka hilo. Au haujawahi kuona mabinti wengine ndani ya kanisa ambalo wamepatia wokovu, wanapoambiwa hayo mavazi mf. Vijisuruali, vinguo vifupi, au night dress za mchana n.k hazikufai wewe uliyeokoka jinsi wanavyopigana na hilo fundisho? Nakwambia huwa  wanathubutu hata kuhama kanisa.
Wengine wakihubiriwa juu ya sadaka, zaka na michango mbalimbali ya kanisa, husema tumechoka na michango na wakati mwingine wanathubutu kuhama makanisa. Wakidhani bado wamo ndani ya ufalme kumbe wanazunguka zunguka nje ya jengo (ufalme wa Mungu) . Inaniuma sana hii.
“Mtumwa hakai nyumbani siku zote” kuna muda anaachiwa achiwa, kuna muda adui akichachamaa anambeba tena na kuondoka naye.
NGOJA TUONE MFANO HUU!!!!!!!
Mbuzi akiwa amefungwa ili ale majani, huwa ni ngumu kujijua kuwa amefungwa, ni mpaka anapotaka kwenda mbali zaidi ya ile kamba ndipo anapoona kamba inamzuia (LIMITATION) lakini kabla, atafurahi, atacheza cheza na kuruka ruka kama wenzake akijua yupo huru. Ila pale tu anapotaka kwenda BEYOND THE ROPE(Umbali zaidi yahiyo kamba/kifungo) ndipo anapojua kuwa amefungwa, anaanza kulia,kujuta na kuhuzunika. Anarudi tena kwenye usawa wa kamba anasahau kidogo machungu na huzuni na anacheza tena na wenzake ( WALIOOKOKA ). Baadae anafikiri tena kwenda BEYOND THE ROPE. Saa hii anatoka kwa spidi, ana hamu ya kula majani yaliyoko beyond the rope; maskini yake anajikuta kamba ina mkaba kwa nguvu anaanguka, kilio, huzuni na maumivu vimemjaa moyoni. Hatari zaidi aliyemfunga kamwona kuwa anataka afanye mbinu za kwenda kula majani na ku enjoy kule beyond the rope, anampa adhabu kali, viboko na mateke. Halafu anamrudisha tena anaendelea na maisha yaleyale ya usawa wa kamba tena kwa mateso maana amemuudhi mfungaji. Kwanini????MTUMWA HAKAI NYUMBANI SIKU ZOTE.
Haya ndiyo maisha waliyoishi wana wa Israeli na tunaona pale Musa anataka kuwaondoa utumwani, ndipo hasira ya Farao ikazidi, akawapa kazi ngumu zaidi na kuwabebesha matofali ya moto. Kutoka 5:1-23. Lakini kwa uaminifu wa Mungu na nguvu zake walipokuwa na utayari wa kukaribisha ufalme wa Mungu ndani yao walifunguliwa kwa maana Bwana alikuwa ana haja nao wakaendelea na safari kueelekea ukombozi na kusudi alilokuwa anataka wakalitimize.
Mwanapunda aliyembeba Yesu alitambua kuwa alikuwa kwenye mateso na utumwa pale tu Yesu alipotuma watu wakamfungue na kuwaambia waliomfunga BWANA ANA HAJA NAYE. Ufahari wa kutembea juu ya nguo za watu na matawi ya mitende hakuwa nao kule kifungoni bali mateso na kubebeshwa mizigo mizito kama waswahili wasemavyo “ PUNDA AFE MZIGO UFIKE” Lakini pale tu alipo kubali kulibeba kusudi la ufalme wa Mungu la kumfikisha Yesu Yerusalemu ndipo anaanza kuheshimiwa kama mwana na siyo mtumwa tena. Luka 19;29-36.
Ukiwa MWANA unakaa nyumbani siku zote. Mwana ni Yule aliye mpokea Yesu. Yohana 1;12. Kumpokea Yesu maana yake; kukubali mafundisho yake, watumishi wake na maonyo yao, kukubali maisha yake (lifestyle) na kuukubali mfumo wa ufalme wa Mungu. Yesu hasimami yeye kama yeye bali akisimama ujue ufalme wake upo. Na mtu pekee atakayestahili kuwa ndani ya ufalme wake ni Yule aliye na utii na kufuata NENO LAKE la sivyo, anakutoa nje ya ufalme. Kumbuka; ufalme una kanuni, taratibu na sheria (BIBLIA).
Sasa turudi kidogo; Ukiwa mwana wa Mungu maana yake umeubeba ufalme wa Mungu na unachukua nafasi ya kifalme. Ufunuo 5;10, Luka 12;32. Katika kitabu cha Mhubiri 8;4 anasema, “….Neno la Mfalme lina nguvu ,naye ni nani awezaye kumwambia wafanya nini?”. Kuna mambo utakuwa wewe ni kuamuru, hautaruhusu adui kufanya bargaining. Mambo mengine siyo hata ya kumlilia Mungu kuwa kwa nini mimi. Yaambie tokaaaa katika jina la Yesuuuu!!!!!!!haleluya!!
Watu wengi wanapenda kuishi kwenye wokovu lakini hawataki kuishika sheria ya wokovu (Sheria ya Roho wa Uzima) inayowafanya  wawe mbali na sheria ya dhambi na Mauti. Warumi 8;2. Ndiyo maana hupendi dhambi lakini unatenda dhambi. Hupendi mauti ya ndoa, uchumba, kazi, elimu, biashara, utakatifu, utumishi, huduma, karama n.k. itokee lakini unajikuta mauti hiyo inakuandama. Kwanini????MTUMWA HAKAI NYUMBANI SIKU ZOTE. Lakini Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kwelikweli.

ITAENDELEA……………..!!!!
IMEANDALIWA NA;-
Mwl. Nickson Kipangula
HUDUMA YA MAOMBI YA UREJESHO
(RESTORATION PRAYERS SERVICE-WORLDWIDE)
SIMU: 0757 350527 (SMS NA WATSAPP)
Blog: www.urejesho.blogspot.com


Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KURUHUSU UTUKUFU (GLORY) WA BWANA KUFANYA JAMBO KATIKA MAISHA YAKO